Malaki 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
7 Munalizarau kwa kunitolea kwenye mazabahu yangu sadaka ya chakula kichafu. Lakini ninyi munauliza: Tumekichafua namna gani? Munakichafua kwa kuizarau mazabahu yangu.
mazabahu ya mbao. Urefu wake kwenda juu ulikuwa metre moja na nusu na upana wa metre moja. Pembe zake, tako lake, na pande zake zote zilikuwa zimetengenezwa kwa mbao. Yule mutu akaniambia hivi: Hii ndiyo meza inayokaa mbele ya Yawe.
Sadaka yoyote ya ngano utakayomuletea Yawe inapaswa kuwa imetengenezwa bila chachu, maana hakuna ruhusa hata kidogo ya kutumia chachu wala asali katika sadaka Yawe anazotolewa kwa moto.
Watakuwa watakatifu kwa Mungu wao wala wasichafue jina la Mungu wao. Maana wao ndio wanaotolea zile sadaka Yawe anazopewa kwa moto, ni kusema chakula cha Mungu. Basi, wanapaswa kuwa watakatifu.
Utamutambua kuhani kuwa aliyetakaswa, maana yeye ndiye anayetolea sadaka ya mukate wa Mungu wako. Utamutambua kuwa mutakatifu, maana mimi Yawe ninayekutakasa wewe ni mutakatifu.
Munasema: Mambo haya yametuchokesha sana na munanizarau. Munaniletea sadaka za nyama muliopata kwa njia ya kunyanganya, au wanaokua vilema au wagonjwa. Basi, nipokee sadaka hizo toka katika mikono yenu?
Munaponitolea sadaka ya nyama anayekuwa kipofu, au kilema, au mugonjwa, huo si uovu? Mutawala atapendezwa au kukutendea mema ukimupa zawadi ya nyama kama yule? –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.