Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe anasema hivi: Nimewapenda ninyi siku zote. Lakini ninyi wazao wa Yakobo munaniuliza: Umetupenda namna gani? Yawe anasema hivi: Si Esau alikuwa ndugu wa Yakobo? Hata hivyo nilimupenda Yakobo

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 1:2
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwambia: “Mataifa mawili yako ndani ya tumbo lako; makabila mawili yatakayozaliwa nawe, yatatengana. Moja litakuwa lenye nguvu kuliko lingine, mukubwa atamutumikia mudogo.”


Wa kwanza alikuwa mwekundu, mwenye nywele mwili wote; hivyo wakamwita Esau.


Wa pili alizaliwa akiwa amemushika Esau kisigino, hivyo wakamupa jina Yakobo. Isaka alikuwa na umri wa miaka makumi sita wakati Esau na Yakobo walipozaliwa.


Hapo Isaka akatetemeka sana, akasema: “Ni nani basi yule aliyewinda na kuniletea nyama ya mawindo, nami nimekwisha kula mbele haujakuja? Tena nimekwisha kumubariki. Hakika, amekwisha kubarikiwa!”


Akaniambia: ‘Nitakufanya ukuwe na wazao na uongezeke. Nitakufanya ukuwe babu ya jamii kubwa za watu. Inchi hii nitawapa wazao wako, wairizi milele.’ ”


Asifiwe Yawe, Mungu wako, ambaye amependezwa nawe, akakuweka juu ya kiti cha kifalme cha Israeli! Kwa sababu Yawe anapenda Israeli milele, amekuweka wewe ukuwe mufalme, kusudi uimarishe haki na sheria ya Mungu.”


Tutashambulia kutokea upande gani?” Yoramu akajibu: “Tutashambulia kutokea jangwa la Edomu.”


Ninyi ni wa bei kali mbele yangu, ninawaheshimu na kuwapenda. Kwa hiyo, ninatoa watu kusudi niwapate ninyi, ninayaachilia mataifa pahali pa maisha yenu.


Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, anayefika kutoka Bosira na nguo ya madoa mekundu? Ni nani huyo aliyevaa nguo ya utukufu, anatembea kwa nguvu zake kubwa? Ni mimi Yawe ninayetangaza ushindi wangu; nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.


Enyi watu! Musikilize vile mimi Yawe ninavyosema: Nimekuwa kama vile jangwa au inchi yenye giza kubwa? Kwa nini basi watu wangu wanasema: Sisi tuko watu huru; hatutakurudilia!


Yawe anasema hivi: Babu zenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu ya bure, hata nao wakakuwa watu bure?


mimi Yawe nilimutokea kwa mbali. Nami nimekupenda kwa mapendo ya milele, kwa hiyo nimeendelea kuwa mwema kwako.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Edomu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamewawinda wandugu zao Waisraeli kwa mapanga, wakaitupilia mbali huruma yao yote ya kindugu. Hasira yao haikuwa na mwisho, waliiacha iwake siku zote.


Mumemuchokesha Yawe kwa maneno yenu matupu. Hata hivyo, munasema: Tumemuchokesha namna gani? Mumemuchokesha munaposema: Yawe anawaona kuwa wazuri watu wanaotenda mabaya; tena anawapenda. Au munapouliza: Yuko wapi yule Mungu mwenye haki?


Lakini kwa kutaka kujipatia haki, yeye akamwuliza Yesu: “Mwenzangu ni nani?”


Hii ndiyo amri ninayowapa: mupendane ninyi kwa ninyi kama ninavyowapenda.


Tena Yawe alifurahia babu zenu kwa kuwapenda na akawachagua ninyi wazao wao pahali pa watu wengine wote, kama hivi leo.


kwa sababu walikataa kuwapatia chakula na maji mulipokuwa katika njia kutoka Misri, na kwa sababu walimulipa Balamu mwana wa Beori kutoka Petori kule Mesopotamia, awalaani.


Yawe anawapenda watu wake, anawalinda watakatifu wake wote. Wanamufuata na kupata maagizo kutoka kwake.


Kwa kuwa aliwapenda wazee wenu, yeye amewachagua ninyi wazao wao, akawatoa yeye mwenyewe katika inchi ya Misri kwa nguvu yake kubwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ