Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 1:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Munasema: Mambo haya yametuchokesha sana na munanizarau. Munaniletea sadaka za nyama muliopata kwa njia ya kunyanganya, au wanaokua vilema au wagonjwa. Basi, nipokee sadaka hizo toka katika mikono yenu?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 1:13
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini mufalme akamwambia Arauna: “Hapana! Wewe hautanipa kitu chochote. Mimi nitavinunua kwako kwa bei yake. Sitamutolea Yawe, Mungu wangu, sadaka za kuteketezwa ambazo sikununua.” Hivyo, mufalme Daudi alinunua kiwanja cha kupepetea na ngombe dume kwa bei ya vikoroti makumi tano vya feza.


Munapokuja mbele yangu kuniabudu, nani aliyewaambia mukanyagekanyage ndani ya viwanja vyangu?


Munachagua mawe laini katika mabonde, na kuyafanya kuwa mungu wenu. Munayamwangia sadaka ya kinywaji na kuyapelekea sadaka ya unga! Mimi nitatulizwa kwa vitu hivyo?


Mimi Yawe ninapenda watu wafuate sheria yangu; ninachukia unyanganyi na uovu. Nitawatunza watu wangu kwa uaminifu, nitafanya nao agano la milele.


Halafu nikamwambia hivi: Ee, Bwana wangu Yawe, sijajichafua hata kidogo kwa kula nyamafu wala nyama aliyeuawa na nyama wa pori, wala sijapata kuonja nyama anayehesabiwa kuwa muchafu tangu ujana wangu.


Makuhani hawatakula nyamafu au ndege yeyote aliyekufa mwenyewe au aliyeraruliwa na nyama wa pori.


Nitawaangamiza, enyi Waisraeli. Nani ataweza kuwasaidia?


Kuhani asikule nyama yoyote ya nyama aliyekufa peke yake au kuuawa na nyama wa pori, kusudi asijichafue. Mimi ni Yawe.


Halafu kisha kubadilisha nguo zake atapeleka yale majivu inje ya kambi pahali panapokuwa safi.


Munajisemesha ndani ya mioyo yenu: Sikukuu ya mwandamo wa mwezi itakwisha wakati gani kusudi tuanze tena kuuzisha vyakula vyetu? Siku ya Sabato itakwisha wakati gani kusudi tupate kuuzisha ngano yetu? Tutapunguza vipimo, tutapandisha bei, tutadanganya watu kwa mizani zisizokuwa sawa.


Anasema hivi: Enyi watu wangu, nimewatendea nini? Nimewachokesha kwa kitu gani? Munijibu!


Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.


Yawe awatenge mbali watu wanaofanya mambo hayo kutoka kati ya wazao wa Yakobo. Na wasishiriki hata kidogo katika kutoa ushuhuda na kuleta sadaka mbele ya Yawe wa majeshi.


Zaidi ya hayo yote, munaifunika mazabahu ya Yawe kwa machozi yenu, mukilia na kuomboleza kwa sababu yeye hazikubali tena sadaka munazomutolea.


“Munapofunga kula chakula, musifanye kama wanafiki, wanaojigeuza kuwa wenye sikitiko na kukunja nyuso zao, kusudi watu waone kwamba wanafunga. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


“Munapoomba, musikuwe kama wanafiki, kwa maana wanapenda kuomba wakisimama katika nyumba za kuabudia na pembeni ya barabara, kusudi wapate kujionyesha mbele ya watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


Lakini nyama huyo akiwa na kilema chochote, ni kusema kiwete au kipofu, au ana kilema chochote kikubwa, usimutoe kuwa sadaka kwa Yawe, Mungu wako.


Kwa nini basi, umezionea wivu matoleo na sadaka nilizowaamuru watu waniletee, nawe ukawaheshimu watoto wako kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu nzuri za sadaka ambazo watu wangu wa Israeli wananitolea?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ