Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 1:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 1:10
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Yawe anasema hivi juu ya watu hawa: Kweli wamependa sana kutangatanga, wala hawakujizuia; kwa hiyo mimi Yawe sipendezwi nao. Sasa nitayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


Hata wakifunga, sitayasikiliza maombi yao, na hata wakinitolea sadaka za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, mimi sitazikubali. Lakini nitawaangamiza kwa vita, njaa na ugonjwa mukali.


Wote, tangu mudogo mpaka mukubwa kabisa, kila mumoja anatamani kupata faida isiyokuwa ya haki. Tangu manabii mpaka makuhani, kila mumoja wao ni mudanganyifu.


Kwa nini kuniletea ubani kutoka Seba, na udi wa harufu nzuri kutoka inchi ya mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto hazikubaliki, wala sadaka zenu zingine hazinipendezi.


Kwa hiyo, wake zao nitawatoa kwa waume wengine, nayo mashamba yao nitawapa wengine. Maana, tangu mudogo mpaka mukubwa, kila mumoja ana tamaa ya faida isiyokuwa ya haki. Tangu manabii mpaka makuhani, kila mumoja anatenda kwa udanganyifu.


Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ngombe, kumutafuta Yawe; lakini hawataweza kumupata, kwa sababu amejitenga nao.


Waamuzi wanahukumu kwa kupewa kutuliro, makuhani wake wanafundisha kwa kupata malipo, manabii wanatabiri kwa kupata feza. Hata hivyo wanajidai kumutegemea Yawe, wakisema: Yawe, si yupo pamoja nasi? Hatutapatwa na hasara yoyote!


Munasema: Mambo haya yametuchokesha sana na munanizarau. Munaniletea sadaka za nyama muliopata kwa njia ya kunyanganya, au wanaokua vilema au wagonjwa. Basi, nipokee sadaka hizo toka katika mikono yenu?


Yawe awatenge mbali watu wanaofanya mambo hayo kutoka kati ya wazao wa Yakobo. Na wasishiriki hata kidogo katika kutoa ushuhuda na kuleta sadaka mbele ya Yawe wa majeshi.


Zaidi ya hayo yote, munaifunika mazabahu ya Yawe kwa machozi yenu, mukilia na kuomboleza kwa sababu yeye hazikubali tena sadaka munazomutolea.


Lakini mutumishi wa mushahara si muchungaji, wala kondoo si wake. Kwa sababu hii wakati anapoona imbwa wa pori anakuja, anaacha kondoo na kukimbia. Na halafu imbwa wa pori anawakamata na kuwasambaza.


Munajua hakika kuwa wale wanaotumika katika hekalu wanapata chakula chao ndani ya hekalu. Na wale wanaotumika kwa kutoa sadaka juu ya mazabahu wanapata sehemu yao kutoka sadaka zile.


Watu wengine wote wanatafuta faida yao wenyewe, lakini hawashuguliki na Yesu Kristo.


Mwenye haki mbele yangu ataishi kwa njia ya imani. Lakini kama akirudi nyuma, sitapendezwa naye.”


Ninawaonya, muchunge lile kundi Mungu alilowapatia, si kwa kulazimishwa, lakini kwa mapenzi yenu sawa vile Mungu anavyotaka. Musitumike kwa ajili ya tamaa mbaya ya mali, lakini kwa kujitoa kwa moyo mwema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ