Luka 9:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
7 Liwali Herode akasikia habari za mambo yote yaliyofanyika. Kwa hiyo akafazaika kwa sababu watu wamoja walikuwa wakisema kwamba Yoane Mubatizaji amefufuka.
Maana leo Yawe wa majeshi ametuletea fujo, kushindwa na wasiwasi katika Bonde la Maono. Kuta za muji zimebomolewa. Kilio cha wakaaji wake kinasikilika mpaka kwenye milima.
Mutu muzuri zaidi kati yao ni kama michongoma, naye mwenye usawa zaidi ni hatari kama upango wa miiba. Siku iliyongojewa ya azabu yao imefika. Na sasa mahangaiko yamewapata.
Nao wakamujibu: “Wamoja wanasema kwamba wewe ni Yoane Mubatizaji; wengine wanasema kwamba wewe ni nabii Elia na wengine wanasema kwamba wewe ni mumoja wa manabii wengine.”
“Vitambulisho vitaonekana katika jua, mwezi na nyota. Na hapa katika dunia mataifa yatakuwa na uchungu, na kushikwa na wasiwasi kwa ajili ya mungurumo na musukosuko wa bahari.
Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Tiberio mufalme wa Roma, Pontio Pilato alikuwa liwali wa jimbo la Yudea, na Herode alikuwa mutawala wa jimbo la Galilaya na ndugu yake Filipo alikuwa mutawala wa inchi ya Iturea na ya Tarakoniti. Vilevile Lisania alikuwa mutawala wa inchi ya Abilene,
Nao wakajibu: “Wamoja wanasema kwamba wewe ni Yoane Mubatizaji, wengine wanasema kwamba wewe ni Elia, na wengine wanasema kwamba wewe ni mumoja wa manabii wa zamani aliyefufuka.”