nasi tukakuelezea kwamba tuko na baba, naye ni muzee, na kwamba tuko na ndugu mwingine mudogo aliyezaliwa wakati wa uzee wa baba yetu. Kaka yake na yule kijana amekwisha kufa, na yule mudogo ndiye peke yake aliyebaki wa mama yake; na muzee wetu anamupenda sana kijana yule.
Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.
Mwanamuke mumoja Mukanana aliyeishi katika pande zile akamufikia, akilalamika, akisema: “Ee Bwana, mwana wa Daudi, unihurumie! Binti yangu anateswa sana na pepo.”
Alipokaribia kwenye mulango wa ukuta wa muji, kukatokea watu wanaobeba maiti ya kijana mumoja aliyekuwa mutoto wa pekee wa mama mumoja mujane. Nao watu wengi wa muji ule walikuwa wakimusindikiza yule mama.
Pepo anapomukamata, mara moja mutoto analalamika, na yule pepo anamutikisatikisa kwa nguvu hata pofu inamutoka. Huyo pepo hatoki ndani yake upesi, naye anamutesa sana.
Wakati aliposikia kwamba Yesu amefika Galilaya toka Yudea, mukubwa huyu akamwendea, akamusihi aende Kapernaumu kumuponyesha mwana wake, aliyekuwa karibu kufa.