Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 9:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Lakini makundi ya watu walipopata habari ile, wakamufuata mpaka kule. Yesu akawapokea na kuanza kusema nao juu ya Ufalme wa Mungu, na vilevile akawaponyesha wale waliohitaji kuponyeshwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 9:11
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


Yesu alipojua habari ile, akaondoka kule. Watu wengi wakamufuata, naye akawaponyesha wagonjwa wote.


Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, naye akawasikilia huruma, akawaponyesha wale waliokuwa wagonjwa kati yao.


Kati ya hawa wawili ni nani aliyefanya sawa na mapenzi ya baba yake?” Wale wakubwa wakajibu: “Ni yule wa kwanza.” Na Yesu akawaambia: “Kweli ninawaambia: Walipishaji wa kodi pamoja na makahaba wataingia mbele yenu katika Ufalme wa Mungu.


Kwa sababu hii ninawaambia: Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa kwa watu watakaotoa matunda yanayostahili ufalme ule. [


Anawatajirisha wenye njaa, lakini amewaacha watajiri mikono mitupu.


Yesu akawajibu: “Wenye afya nzuri hawahitaji muganga, lakini wale wanaokuwa wagonjwa.


Nyuma ya pale Yesu akapita katika miji na vijiji mbalimbali, akihubiri na kutangaza Habari Njema ya Ufalme wa Mungu. Wale wanafunzi wake kumi na wawili walienda naye


Akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa Mungu, lakini kwa watu wengine si vile. Wao wanaambiwa maneno hayo kwa njia ya mifano, kusudi waangalie, lakini wasione kitu, nao wasikie, lakini wasifahamu kitu.”


Mitume waliporudia toka kuhubiri wakamwelezea Yesu mambo yote waliyofanya. Kisha akaondoka pamoja nao na kwenda kwenye nafasi ya upekee karibu na muji Betesaida.


Jua lilipoanza kushuka, wanafunzi kumi na wawili wa Yesu wakamufikia na kumwambia: “Hapa tunapokuwa ni katika pori. Uage makundi haya ya watu kusudi waende katika vijiji vinavyokuwa hapa karibu na kwenye nyumba kule katika mbuga kwa kujitafutia chakula na nafasi ya kulala.”


Halafu akawatuma kuhubiri habari za Ufalme wa Mungu na kuwaponyesha wagonjwa,


Yesu akawaambia: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya yule aliyenituma na kutimiza kazi yake.


Wote Baba anaonipa wanakuja kwangu; nami sitamukataa hata kidogo yule anayekuja kwangu.


Alihubiri habari za Ufalme wa Mungu na kuwafundisha watu juu ya Bwana Yesu Kristo bila woga na bila kuzuizwa.


Basi namna gani watamusihi yule wasiyemwamini? Na namna gani watamwamini yule wasiyesikia habari zake? Na namna gani watasikia habari zake ikiwa hakuna wanaohubiri?


Hivi basi imani inatokana na kusikia habari, na habari ile inatokana na neno la Kristo.


Kwa maana hata Kristo hakufanya mambo yanayomupendeza mwenyewe sawa vile ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Matusi wanayokutukana, yananiangukia.”


utangaze Neno la Mungu kwa nguvu kwa wakati unaofaa na kwa wakati usiofaa. Ukaripe, usahihishe na kuonya ukifundisha kwa uvumilivu.


Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ