Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 8:52 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

52 Watu wote walikuwa wakilia na kusikitika sana kwa ajili ya kifo cha mutoto. Lakini Yesu akasema: “Musilie, kwa maana hakufi, lakini analala tu!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 8:52
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alikufia kule Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya Kanana. Abrahamu akaomboleza na kumufanyia Sara muke wake kilio.


Utukufu wa Yawe ukaonekana mbele ya macho ya watu wa Israeli kama moto unaowaka juu ya mulima.


Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.


‘Tuliwapigia ngoma, lakini hamukucheza! Tuliimba wimbo wa kilio, lakini hamukulia!’


Kundi kubwa la watu walimufuata. Kati yao kulikuwa wanawake waliokuwa wakijipigapiga kwenye kifua kwa huzuni na kumulilia.


Nalo kundi la watu waliofika kuangalia mambo yale, wakaona yote yaliyotokea. Kwa hiyo, wakarudia wakijipigapiga kwenye kifua kwa huzuni.


Yesu alipofika ndani ya nyumba ya Yairo, hakuruhusu mutu kuingia pamoja naye isipokuwa Petro, Yoane, Yakobo, baba na mama wa mutoto.


Nao wakamuchekelea kwa sababu walijua kwamba amekwisha kufa.


Wakati Yesu aliposikia habari hii, akasema: “Tukio la ugonjwa huu si la kumwua, lakini shabaha yake ni kuonyesha utukufu wa Mungu na kusudi Mwana wa Mungu atukuzwe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ