Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 8:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Na karibu na pale kulikuwa kundi la nguruwe wengi waliokuwa wakijitafutia chakula kwenye mulima. Wale pepo wakamusihi Yesu awaruhusu kuingia ndani ya wale nguruwe. Naye akawaruhusu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 8:32
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwuliza: ‘Kwa namna gani?’ Naye akajibu: ‘Nitakwenda na kuwasukuma manabii wake wote waseme uongo.’ Yawe akamwambia: ‘Wewe utamushawishi na utashinda; basi, kwenda ufanye hivyo.’


Si wewe mwenyewe unamulinda pande zote pamoja na jamaa yake na kila kitu anachokuwa nacho? Wewe umemubariki na mali yake imeongezeka katika inchi.


Yawe akamwambia Shetani: “Basi, unaweza kufanya vile unavyotaka juu ya mali yake. Lakini tu yeye mwenyewe usimuguse.” Basi, Shetani akaondoka mbele ya Yawe.


Yawe akamwambia Shetani: “Basi, unaweza kumufanya vile unavyotaka, lakini usimwue tu.”


Musitegemee kutesa, musijisifie mali ya wizi; kama mali zikiongezeka, musizitegemee.


Wanaikaa katika makaburi na kupitisha usiku ndani ya mashimo. Wanakula nyama ya nguruwe na kuweka muchuzi wa nyama wachafu ndani ya sahani zao.


Lakini watu hawa wanafanya wanavyotaka: wananitolea sadaka ya ngombe na tena wanaua watu kwa kutambikia. Wananitolea sadaka ya mwana-kondoo na vilevile wanaua imbwa. Wananitolea sadaka ya unga na vilevile wanatolea damu ya nguruwe. Wanachoma ubani mbele yangu na kwenda kuabudu miungu ya uongo. Hao wamechagua kufuata njia zao wenyewe.


Musikule nguruwe. Yeye ana kwato zinazogawanyika lakini hacheui. Kwenu huyo ni muchafu.


“Musiwape imbwa vitu vitakatifu, kusudi wasiwageukie na kuwararua, wala musiwatupie nguruwe ushanga zenu za bei kusudi wasizikanyagekanyage.


Nao wale pepo walimusihi Yesu kwamba atakapowafukuza asiwaamuru kutumbukia ndani ya shimo lisilokuwa na mwisho.


Basi pepo wakamutoka mutu yule na kuingia ndani ya wale nguruwe. Kundi zima la nguruwe wakatelemuka mbio kwenye mulima na kutumbukia ndani ya maji, nao wakazama.


Yesu akamujibu: “Wewe hauna mamlaka yoyote juu yangu, isipokuwa tu yale uliyopewa na Mungu toka juu. Ni kwa hiyo, yule aliyenitoa kwako anabeba zambi kubwa zaidi.”


Lakini ninyi, watoto wangu, muko watoto wa Mungu, nanyi mumewashinda manabii wa uongo; maana roho anayekaa ndani yenu ni mwenye uwezo kuliko yule anayekaa ndani ya watu wa dunia.


Wakati ile miaka elfu moja itakapotimia, Shetani atafunguliwa toka katika kifungo chake,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ