Halafu akawaambia wanafunzi wake: “Imani yenu iko wapi?” Nao wakaogopa na kushangaa, wakiulizana: “Huyu ni mutu gani? Anaamuru hata zoruba na ziwa, navyo vinamutii!”
Yesu alipotoka ndani ya chombo, akakutana na mutu mumoja kule katika muji aliyeshikwa na pepo. Mutu yule hakuvaa nguo tangu siku nyingi, wala hakuishi ndani ya nyumba, lakini aliishi kwenye makaburi.