Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 8:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 “Basi mufanye angalisho na jinsi munavyosikia maneno. Kwa maana mutu anayekuwa na kitu, ataongezewa kingine, lakini mutu asiyekuwa na kitu, atanyanganywa kile anachozania kuwa nacho.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 8:18
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kuna njia inayozaniwa kuwa sawa, lakini kwa mwisho inaongoza kwenye kifo.


Kwa maana mutu anayekuwa na kitu ataongezewa kingine, naye atakuwa na vitu vingi. Lakini mutu asiyekuwa na kitu, ataondolewa hata kile kidogo anachokuwa nacho.


Kwa maana mutu anayekuwa na kitu ataongezewa kingine; lakini mutu asiyekuwa na kitu, ataondolewa hata kidogo anachokuwa nacho.


“Lakini mutamwona yule anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ akisimamishwa pahali asipopaswa kuwa. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake). Basi watakaokuwa Yudea, wakimbilie kwa milima.


Akawajibu: ‘Ninawaambia kwamba mutu anayekuwa na kitu ataongezewa kingine, lakini mutu asiyekuwa na kitu ataondolewa hata kidogo anachokuwa nacho.


“Munitegee sikio vizuri: Mwana wa Mutu atatolewa katika mikono ya watu.”


Yeye anakata kila tawi linalokuwa ndani yangu lisilozaa matunda. Naye anasafisha kila tawi linalozaa matunda, kusudi lizae matunda mengi zaidi.


Na pale pale nikatuma watu kwako, nawe umefanya vizuri kwa kufika. Sasa sisi wote tuko hapa mbele ya Mungu kwa kusikiliza mambo yote Bwana aliyokuagiza kutuambia.”


Watu hao walikuwa wenye nia nzuri zaidi kuliko watu wa Tesalonika; nao walipokea Neno la Mungu kwa hamu kubwa. Kila siku walichunguza Maandiko Matakatifu wapate kujua kwamba maneno Paulo aliyosema yalikuwa ya haki.


Kufuatana na neema niliyopewa na Mungu, ninawaambia ninyi wote: mutu asijiwazie kuwa na ukubwa kupita vile inavyomustahili. Lakini mukuwe na mawazo ya ukadirifu, kila mumoja kulingana na kipimo cha imani aliyopewa na Mungu.


Kama mutu akizani kwamba yuko na zawadi ya unabii au zawadi ingine ya Roho, anapaswa kujua kwamba maneno haya ninayowaandikia ninyi ni amri ya Bwana.


Mutu yeyote asijidanganye mwenyewe. Kama mutu fulani kati yenu akijizania kuwa mwenye hekima ya kidunia, ajifanye kama mupumbafu kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.


Kama mutu anajizania kwamba anajua kitu, yeye hakijui hakika sawa vile inavyomupasa kukijua.


Lakini mimi vilevile niko na haki ya kuweka tumaini katika mambo ya kimwili. Kama kuna mutu anayejizania kuwa na sababu ya kutumainia mambo ya kimwili, mimi ninamupita.


Kwa sababu hiyo, tunapaswa kushikamana zaidi na habari tuliyosikia, kusudi tusipotee mbali.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ