Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 8:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Nao udongo muzuri walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na kwa uhaki. Ndio wale wanaovumulia hata wanatoa matunda mazuri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 8:15
40 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nimeshika neno lako ndani ya moyo wangu, kusudi nisikukosee.


Unijaze furaha na shangwe, unifurahishe tena, mimi ambaye uliniponda.


Mwana wangu, usisahau mafundisho yangu, lakini kwa moyo wako ushike amri zangu.


Palepale maneno yako yaliponifikia, niliyameza; nayo yakanifurahisha, yakakuwa matamu katika moyo wangu, maana mimi ninajulikana kwa jina lako, ee Yawe wa majeshi.


Kisha siku hizo, nitafanya agano hili na Waisraeli. Nitaiweka sheria yangu ndani yao, na kuiandika katika mioyo yao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Wakaldea wanaoushambulia muji huu wataingia na kuuteketeza kwa moto; watauteketeza pamoja na nyumba ambazo juu ya paa zake ubani ulifukiziwa kwa mungu Bali na sadaka za divai zilitolewa kwa miungu mingine, kwa kunichokoza.


Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ataokolewa.


Lakini Yesu akajibu: “Heri zaidi wale wanaosikia neno la Mungu na kulitii!”


Mutu muzuri anasema maneno mazuri kutokana na uzuri wa moyo wake. Na mutu mubaya anasema maneno mabaya kutokana na ubaya wa moyo wake. Kwa maana kinywa cha mutu kinasema maneno yanayojaa ndani ya moyo wake.


Na mbegu zilizoanguka katika miiba ni mufano wa wale wanaosikia, lakini masumbuko, utajiri na raha ya dunia vinawasonga hata wanashindwa kutoa matunda yanayokomaa.


“Hakuna mutu anayewakisha taa na kuifunika na chombo fulani au kuiweka chini ya kitanda. Lakini anaiweka juu ya kinara kusudi wanaoingia ndani wapate kuona mwangaza.


“Kama munanipenda, mutashika amri zangu.


Kama mukishika amri zangu, mutakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba yangu na kukaa katika upendo wake.


Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.


Lakini sasa kufuatana na vile mumewekwa huru toka utawala wa zambi na kugeuka watumwa wa Mungu, munapata faida ya kuishi katika utakatifu na kwa mwisho kupewa uzima wa milele.


Kwa maana ninajua kwamba hakuna kitu kizuri kinachokaa ndani yangu, ni kusema katika hali yangu ya kimwili. Ni hivi kwa sababu ninakuwa na utashi wa kufanya jambo jema, lakini sifikii kulifanya.


Nanyi wandugu zangu, ni hivi inavyokuwa kwa ngambo yenu. Kufuatana na maneno ya Sheria, ninyi vilevile mumekufa, kwa maana muliungana na mwili wa Kristo. Na sasa munakuwa wa mutu mwingine, ndiye yule aliyefufuka, kusudi tupate kufanya matendo yanayofaa katika kazi ya Mungu.


Lakini tukitumainia kitu tusichokiona, tunakingojea kwa uvumilivu.


Kutahiriwa au kutotahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni kutii amri za Mungu.


Kwa maana mumeokolewa kwa neema ya Mungu, kwa njia ya imani. Jambo hili halitokani na ninyi wenyewe, lakini ni zawadi ya Mungu.


Yawe, Mungu wenu, atawafanya ninyi na wazao wenu mukuwe na moyo wa utii kusudi mumupende yeye kwa moyo wenu wote na roho yenu, mupate kuishi.


Maisha yenu yatajazwa matendo ya haki ambayo Yesu Kristo anayowajalia, kwa ajili ya utukufu na sifa ya Mungu.


Hivi, mutaweza kuishi sawa Bwana anavyotaka na kumupendeza katika mambo yote. Kwa njia hiyo mutafikia kufanya matendo mema ya kila namna na kuzidi kumujua Mungu.


Habari Njema ile inatoa matunda na kuenea katika dunia yote sawa vile ilivyofanya kwenu tangu siku ile muliposikia wakisema juu ya neema ya Mungu na kupata kuitambua inavyokuwa kweli.


Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.


Kwa sababu hiyo, tunapaswa kushikamana zaidi na habari tuliyosikia, kusudi tusipotee mbali.


Lakini sherti uvumilivu ule utimize kazi yake, kusudi mupate kuwa wakamilifu na watimilifu wasiopungukiwa na kitu.


Sisi tunatambua kwamba tunamujua Mungu ikiwa tunashika amri zake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ