Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 7:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Hata mimi vilevile ni mutu mwenye kuwa chini ya mamlaka ya wakubwa, na tena niko na waaskari wengine wanaokuwa chini yangu. Nami nikimwambia mumoja: ‘Kwenda!’ naye anakwenda! Nikimwambia mwingine: ‘Kuja!’ naye anakuja! Nami nikimwambia mutumishi wangu: ‘Fanya hivi!’ naye anafanya vile!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 7:8
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ndiyo sababu nilijiona kwamba sistahili kuja kwako. Lakini sema neno tu, na mutumishi wangu atapona.


Yesu aliposikia maneno haya, akashangaa sana na yule mukubwa, na kugeukia kundi la watu waliomufuata, na kusema: “Ninawaambia: katika inchi yote ya Israeli sijaona bado mutu anayekuwa na imani kubwa kama huyu.”


Basi Paulo akaita mumoja wa wakubwa wa waaskari na kumwambia: “Umupeleke kijana huyu kwa jemadari kwa maana yuko na neno la kumwambia.”


Kisha jemadari akawaita wakubwa wawili wa waaskari wake, akawaambia: “Mutayarishe waaskari mia mbili, waaskari wapanda-farasi makumi saba, na waaskari wapiga mikuki mia mbili kwa kwenda Kaisaria saa tatu ya usiku.


“Mimi Klaudio Lusia, ninakuandikia wewe muheshimiwa Liwali Feliki, pokea salamu zangu.


Basi wale waaskari wakafanya kama vile walivyoamuriwa. Wakamutwaa Paulo, na usiku ule ule wakamufikisha mpaka Antipatiri.


Kisha akamwamuru yule mukubwa wa jeshi kwamba wamulinde Paulo katika kifungo wakimwachia uhuru kidogo, na wasiwazuize warafiki zake kumusaidia.


Mimi sina maneno kamili ya kumwandikia Mufalme wa Roma juu yake. Ndiyo maana nimemuleta mbele yenu na zaidi mbele yako, wewe mufalme Agripa, kusudi kisha kumwuliza, nipate maneno ya kuandika.


Ninyi watumwa, muwatii wabwana wenu katika mambo yote hapa katika dunia. Musiwatii tu wakati wanapowaangalia ninyi kama mungetaka tu kujipendeza mbele yao, lakini muwatii kwa moyo mwema, kwa sababu munamuheshimu Bwana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ