Watu wote wakashangaa sana na kuulizana: “Hatujaona mambo kama haya! Hakika mafundisho haya ni yenye mamlaka! Mutu huyu anaamuru hata pepo, nao wanamutii!”
Halafu Yesu akaenda pamoja nao. Alipokuwa karibu na kwa yule mukubwa wa waaskari, yule mukubwa akawatuma warafiki zake kumwambia Yesu: “Bwana, usijisumbue, kwa maana mimi sistahili kukupokea ndani ya nyumba yangu.
Hata mimi vilevile ni mutu mwenye kuwa chini ya mamlaka ya wakubwa, na tena niko na waaskari wengine wanaokuwa chini yangu. Nami nikimwambia mumoja: ‘Kwenda!’ naye anakwenda! Nikimwambia mwingine: ‘Kuja!’ naye anakuja! Nami nikimwambia mutumishi wangu: ‘Fanya hivi!’ naye anafanya vile!”
Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.