Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 7:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Halafu Yesu akaenda pamoja nao. Alipokuwa karibu na kwa yule mukubwa wa waaskari, yule mukubwa akawatuma warafiki zake kumwambia Yesu: “Bwana, usijisumbue, kwa maana mimi sistahili kukupokea ndani ya nyumba yangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 7:6
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Yakobo akamwomba Mungu akisema: “Ee Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu wa baba yangu Isaka! Ewe Yawe uliyeniambia nirudi katika inchi yangu kwa jamaa yangu, ukaniahidi kunitendea mema,


Kiburi cha mutu kinamuzaraulisha mwenyewe, lakini munyenyekevu wa roho atapata heshima.


Kwa maana Mwana wa Mutu hakukuja kutumikiwa, lakini kutumikiana na kutoa maisha yake kusudi awakomboe watu wengi.”


Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.


Basi Yesu akaenda pamoja naye. Watu wengi walimufuata na kumusongasonga.


Simoni Petro alipoona mambo hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu na kusema: “Bwana, utoke karibu nami, kwa sababu mimi ni mutu mwenye zambi!”


Wale wasimamizi walipofika kwa Yesu, wakamusihi sana, wakasema: “Umufanyie mutu huyu sawa anavyokuomba, kwa maana anastahili kutendewa vile.


Yeye anapenda taifa letu na ni yeye aliyetujengea nyumba yetu ya kuabudia.”


Ndiyo sababu nilijiona kwamba sistahili kuja kwako. Lakini sema neno tu, na mutumishi wangu atapona.


Yesu alipokuwa hajamaliza kusema maneno hayo, mujumbe mumoja akafika toka kwa yule mukubwa Yairo wa nyumba ya kuabudia na kumwambia: “Binti yako amekwisha kufa. Usiendelee kumusumbua Mwalimu.”


Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.


Mujinyenyekeze mbele ya Bwana, naye atawainua.


Lakini Mungu ametujalia neema kubwa zaidi, kwa maana Maandiko yanasema: “Mungu anapingana na wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ