Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 7:44 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

44 Halafu akamugeukia yule mwanamuke na kumwambia Simoni: “Unamwona mwanamuke huyu? Niliingia ndani ya nyumba yako, nawe haukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini mwanamuke huyu amenawa miguu yangu na machozi yake na kuipanguza na nywele zake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 7:44
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutaletewa maji kidogo kusudi munawe miguu na kupumzika chini ya muti.


Akasema: “Bwana zangu, karibu katika nyumba yangu mimi mutumishi wenu. Munaweza kunawa miguu na kulala kwangu usiku wa leo. Asubui mapema mutaweza kuendelea na safari yenu.” Lakini, wao wakasema: “Hapana! Sisi tutalala huku katika barabara.”


Yule musimamizi alipowakaribisha ndani ya nyumba kwa Yosefu, akawapa maji ya kunawa miguu yao, na punda wao akawakulisha.


Halafu Daudi alimwambia Uria: “Urudie kwako unawe miguu yako.” Uria alitoka kwa mufalme, na mara moja mufalme akamupelekea zawadi.


Akakuja kuinama kwenye miguu ya Yesu, akilia. Machozi yake yakamwangika juu ya miguu ya Yesu, akaipanguza na nywele zake, akaibusu na kuipakaa marasi.


Simoni akajibu: “Ninazani kwamba ni yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi.” Na Yesu akamwambia: “Umejibu vizuri.”


Kisha akatia maji ndani ya bakuli, na kuanza kunawisha miguu ya wanafunzi wake na kuipanguza na kile kitambaa alichokifunga katika kiuno.


Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.


Lakini ninyi munawazarau wamasikini! Watajiri si ndio wale wanaowagandamiza ninyi na kuwashitaki kwenye tribinali?


Hivyo akawapeleka katika nyumba yake na kuwapa punda wao malisho. Hao wasafiri wakanawa miguu yao, wakakula na kunywa.


Abigaili alisimama, na kuinama mbele yao uso mpaka chini, akasema: “Mimi ni mujakazi tu. Niko tayari kunawisha miguu ya watumishi wa bwana wangu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ