Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 7:40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

40 Yesu akamwambia yule Mufarisayo: “Simoni, niko na neno la kukuuliza.” Simoni akajibu: “Mwalimu, sema.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 7:40
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini, nina jambo moja tu la kukuambia.” Batiseba akamwambia: “Sema tu.”


Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoto anamuheshimu muzazi wake, na mutumishi anamuheshimu bwana wake. Ikiwa mimi ndiye Baba wenu, mbona munanivunjia heshima? Ikiwa mimi ni bwana wenu, mbona hamuniheshimu? Ninasema hivyo kwa ninyi makuhani munaozarau jina langu. Nanyi munauliza: Sisi tumezarau jina lako namna gani?


Yuda alipofika, akamujongelea Yesu, na kumwambia: “Jambo, Mwalimu.” Na kisha akamubusu.


Siku ile ya hukumu itakapotimia, wengi wataniambia: ‘Bwana, Bwana, sisi hatukutangaza ujumbe wa Mungu? Nasi hatukufukuza pepo kwa jina lako na kufanya maajabu mengi kwa jina lako?’


Mutawala mumoja akamwuliza Yesu: “Mwalimu mwema, nifanye nini kusudi nipate uzima wa milele?”


Halafu Yesu akitambua mafikiri yao, akawauliza: “Sababu gani munajiuliza mambo hayo yote?


Yesu akawajibu: “Wenye afya nzuri hawahitaji muganga, lakini wale wanaokuwa wagonjwa.


Lakini kwa kuwa Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mutu mwenye mukono unaokauka: “Simama pale mbele ya watu.” Naye akaenda kusimama pale.


Yule Mufarisayo aliyemwalika Yesu alipoona vile, akajisemesha: “Kama mutu huyu angekuwa kweli nabii, angetambua mwanamuke huyu anayemugusa ni wa namna gani. Angetambua kwamba yeye ni mwenye mwenendo mubaya.”


Yesu akasema: “Kulikuwa watu wawili waliokopesha feza kutoka kwa mutu mumoja. Mumoja alikuwa na deni ya vikoroti mia tano vya feza na mwingine vikoroti makumi tano.


Munaniita ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ na munasema kweli, maana ni vile ninavyokuwa.


Yesu alitambua kwamba walitaka kumwuliza. Basi akawaambia: “Munaulizana juu ya maneno niliyosema kwamba kunabaki wakati kidogo nanyi hamutaniona, lakini kisha wakati kidogo mutaniona tena?


Sasa tunajua kwamba unajua yote na si lazima mutu akuulize kitu. Sababu hii tunaamini kama ulitoka kwa Mungu.”


Alimwendea Yesu usiku na kumwambia: “Mwalimu, tunajua kama Mungu amekutuma kufundisha, kwa maana hakuna mutu anayeweza kuonyesha vitambulisho hivi unavyoonyesha isipokuwa anaongozwa na Mungu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ