Ninawaambia: kati ya watu wanaoishi katika dunia, hakuna anayekuwa mukubwa kuliko Yoane. Lakini yeyote anayehesabiwa kuwa mudogo katika Ufalme wa Mungu anahesabiwa kuwa mukubwa kuliko yeye.”
Mutu huyu alikuwa amefundishwa Njia ya Bwana, naye alitangaza kwa bidii sana na kufundisha kwa ukweli habari za Yesu. Lakini alikuwa akijua tu ubatizo wa Yoane.
Hawakufahamu namna Mungu anavyowahesabia watu haki na wakatafuta kusimamisha haki yao wenyewe. Wakakataa kufuata njia ya kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.
Waliimba wimbo wa Musa, mutumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana- Kondoo wakisema: “Ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makubwa na ya ajabu! Ewe Mufalme wa mataifa, kazi zako ni za haki na za kweli!
Adoni-Bezeki akasema: “Wafalme makumi saba waliokatwa vidole gumba vya mikono na miguu waliokota makombo chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa kama nilivyotenda.” Wakamupeleka Yerusalema, akakufia kule.