“Ikiwa kuna njaa katika inchi, au ugonjwa mukali, ukosefu wa mvua, ugonjwa wa mimea, nzige au vidudu vingine, au ikiwa watu wako wameshambuliwa na waadui zao katika muji wao wowote, ikiwa kuna pigo lolote au ugonjwa wowote,
Lakini ikiwa kisha kuchunguza nyumba hiyo, kuhani akiona kwamba taka halikuenea kisha kupigwa lipu, basi, kuhani atatangaza kwamba nyumba hiyo ni safi maana taka limekwisha.
Yesu alizunguka katika Galilaya yote akifundisha katika nyumba zao za kuabudia, akihubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha watu waliokuwa na magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.
Habari zake zikavuma katika inchi yote ya Suria. Wakamuletea watu wote walioteswa na magonjwa mbalimbali na wenye maumivu ya kila namna, wenye pepo, wenye kifafa na wenye kupooza, naye Yesu akawaponyesha.
Wale wanafunzi walipofika kwa Yesu wakamwambia: “Yoane Mubatizaji ametutuma kwako kukuuliza ikiwa wewe ndiwe yule aliyepaswa kuja au tumungojee mwingine.”