Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 6:48 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

48 anafananishwa na mutu aliyejenga nyumba, akaichimbia musingi chini sana mpaka kwenye jiwe, na kuujenga pale. Mvua kubwa iliponyesha, muto ukajaa na maji yakashambulia nyumba ile, lakini hayakuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 6:48
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alisema: Yawe ni: kikingio changu, kimbilio langu, mukombozi wangu,


Nani anayekuwa Mungu isipokuwa Yawe? Nani anayekuwa kikingio isipokuwa Mungu wetu?


Yawe anaishi! Asifiwe yeye kikingio changu! Atukuzwe Mungu, kikingio na mwokozi wangu.


Mawimbi ya kifo yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinishambulia,


Mungu wa Israeli amesema, Yeye Jiwe la Kufichamia la Israeli ameniambia: Mutu anayetawala watu kwa haki, anayewatawala akimwogopa Mungu,


Kwa hiyo, kila mwaminifu akutolee maombi wakati wa taabu. Mafuriko ya maji hayatamufikia.


Kwa Mungu peke yake ninapata utulivu, wokovu wangu unatoka kwake.


Mukuje tumwimbie Yawe, tumushangilie yeye kikingio na mwokozi wetu!


Upepo mukali unapopita na mwovu anatoweka, lakini mwenye haki anaimarishwa milele.


Mutumainie Yawe siku zote kwa maana yeye ni kikingio chetu kwa milele.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.


Toka magaribi mpaka mashariki, kila mutu atamwogopa Yawe na kutambua utukufu wake. Maana atakuja kama muto wenye kuporomoka mbio, muto unaosukumwa kwa upepo wa Yawe.


Waadui wakishambulia inchi kama mafuriko, yeye anawaangamiza; anawafuatilia na kuwafukuza mpaka katika giza.


Nitawaonyesha mufano wa mutu anayenifuata, anayesikia maneno yangu na kuyashika:


Lakini yule anayesikia maneno yangu pasipo kuyashika, anafananishwa na mutu aliyejenga nyumba juu ya udongo bila kuchimba musingi. Maji kutoka muto yakaishambulia, na mara moja ikaanguka na kubomoka kabisa.”


Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Ninyi vilevile ni kama jengo linalosimama juu ya musingi uliowekwa na mitume na manabii; Yesu Kristo mwenyewe ndiye jiwe kubwa la pembe.


Watu wa usawa walinona, wakapiga mateke. Walinenepa sana, kisha wakamwacha Mungu aliyewaumba, wakazarau Mulima wa wokovu wao.


Hamukumujali Mulima wenu, yule aliyewapa uzima. Mulimusahau Mungu aliyewazaa ninyi.


Hata waadui zetu wenyewe wanajua wazi, mulinzi wao hana nguvu kama mulinzi wetu.


Lakini musingi uliojengwa na Mungu, unasimama imara. Nayo maneno haya yamechapwa juu ya musingi ule “Bwana anajua wale wanaokuwa wake,” na haya mengine: “Kila mutu anayesema kwamba yeye ni wa Bwana anapaswa kujitenga na maovu.”


Kwa hiyo wandugu zangu, kufuatana na vile mulivyochaguliwa na kuitwa na Mungu, mufanye nguvu zaidi kwa kukamilika katika njia ile. Mukitenda mambo yale hamutaanguka hata kidogo.


Na sasa watoto wangu, mukae ndani yake kusudi tukuwe na tumaini hakika wakati atakapotokea, na kutosikia haya mbele yake siku atakaporudi.


Basi yeye anayeweza kuwalinda kusudi musianguke, na kuwasimamisha ninyi mbele ya utukufu wake pasipo kilema na kwa furaha kubwa,


Hakuna anayekuwa mutakatifu kama Yawe; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye; hakuna anayekuwa jiwe la kufichamia kama Mungu wetu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ