Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 6:41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

41 “Namna gani unaona vumbi inayokuwa ndani ya jicho la ndugu yako, lakini haufikiri juu ya nguzo inayokuwa ndani ya jicho lako?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 6:41
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu atamwazibu Yoabu kwa mauaji hayo aliyoyafanya bila baba yangu kuwa na habari. Yeye aliwaua watu wawili ambao walikuwa wa maana zaidi kuliko yeye, tena walimupita kwa wema; aliwaua Abeneri mwana wa Neri, jemadari wa kundi la waaskari Waisraeli, na Amasa mwana wa Yeteri, jemadari wa waaskari wa Yuda.


Lakini Yoabu hakuwahesabu Walawi na watu wa kabila la Benjamina, kwa sababu alichukizwa sana na amri ya mufalme.


Zambi inaongea na mutu mwovu, ndani kabisa ya moyo wake; kuogopa Mungu si kitu kwake.


Moyo wa mutu ni mudanganyifu kuliko vitu vyote; hauwezi kuponyeshwa, hakuna anayeweza kuuelewa!


Kwa sababu amefikiri, akaachana na makosa aliyoyafanya, hakika ataishi; hatakufa.


“Musiwahukumu wengine kusudi Mungu asiwahukumu ninyi vilevile.


Walikuwa vilevile na samaki ndogo chache. Yesu akamushukuru Mungu na kuwaambia wanafunzi wazigawanye vilevile.


Mwanafunzi hamupiti mwalimu wake akili, lakini kila mwanafunzi anayetimiza mafundisho yake, atakuwa kama mwalimu wake.


Au, namna gani unaweza kumwambia ndugu yako kwamba aache umwondoe vumbi inayokuwa ndani ya jicho lake, wakati ndani ya jicho lako mungali ile nguzo. Wewe munafiki, ondosha kwanza nguzo kutoka ndani ya jicho lako, kisha utaweza kuona waziwazi na kuweza kuondosha ile vumbi inayokuwa ndani ya jicho la ndugu yako.


Nao walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka na kuwaambia: “Mutu asiyekuwa na zambi kati yenu, akuwe wa kwanza kumutupia jiwe.”


Wewe unayemuhukumu mwingine hauna namna yoyote ya kujitetea, haizuru wewe ni nani. Kwa maana wakati unapohukumu mwingine, unajikatia hukumu wewe mwenyewe, kwa sababu wewe unayehukumu unatenda mambo yale yale.


Kisha kujiangalia, anajiendea, na mara moja anasahau namna anavyokuwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ