“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munasafiri kuvuka bahari na inchi mbalimbali kusudi mupate kumugeuza hata mutu mumoja tu kuwa mufuasi wenu. Nanyi munapomupata, munamufanya kuwa mwenye kustahili azabu ya jehenamu mara mbili zaidi kuliko ninyi.
Mukumbuke maneno niliyowaambia kwamba mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake. Kama walinitesa mimi, watawatesa ninyi vilevile. Na kama walishika maneno yangu, watashika maneno yenu vilevile.