Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 6:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Yesu akawaambia tena wanafunzi wake mufano huu akiwauliza: “Kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwingine? Wote wawili hawatatumbukia ndani ya shimo?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 6:39
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana walinzi wa Israeli wote ni vipofu; wote hawana akili yoyote. Wote ni kama imbwa bubu wasioweza kufoka, wanalala tu na kuota ndoto, wanapenda sana kusinzia!


Kwa hiyo, Yawe hawahurumii vijana wao, hana huruma juu ya wayatima na wajane wao; maana hakuna hata mumoja anayemufuata, kila mutu anasema upumbafu. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Wao walisikia haya walipofanya machukizo hayo? Hapana! Hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo wataanguka pamoja na wale wanaoanguka; wakati nitakapowaazibu, wataangamizwa kabisa. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Walisikia haya walipotenda machukizo hayo? Hapana, hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka; nitakapowaazibu, wataangamia. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Halafu akawafundisha mambo mengi akitumia mifano, akasema: “Mutu mumoja alikwenda kupanda mbegu.


Muwaache! Wao ni vipofu, wanaongoza vipofu wengine. Na kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili wanatumbukia ndani ya shimo.”


Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani mutaweza kuepuka azabu ya jehenamu?


Unajiaminia kwamba wewe ni mwongozi wa vipofu na mwangaza kwa wale wanaokuwa katika giza,


Lakini watu waovu na wadanganyifu wataendelea katika maovu, wakipotosha watu wengine na kujipotosha wenyewe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ