Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 6:38 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

38 Muwape wengine, na Mungu atawapa ninyi. Mutapokea kipimo kikubwa kilichojaa zaidi. Kwa maana mutapimiwa na kipimo kile munachotumia kwa wengine.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 6:38
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mimi leo nina umri wa miaka makumi nane. Niko na uwezo wa kutambua yanayokuwa mazuri na yale yasiyokuwa mazuri? Mimi mutumishi wako ninaweza tena kutambua onjo ya kile ninachokula au kunywa? Nitaweza tena kutambua uzuri wa sauti za waimbaji wanaume au wanawake? Kwa nini mimi mutumishi wako nikuwe muzigo wa zaidi kwako bwana wangu mufalme?


Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.


Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.


Kisha wandugu zake, wadada zake na warafiki wote waliomufahamu mbele wakamwendea kwake, wakakula chakula pamoja naye. Wakamupa pole na kumufariji kwa ajili ya mateso yote ambayo Yawe alikuwa amemuletea. Kila mumoja wao akamupa Yobu feza na pete ya zahabu.


Ee Bwana, uwalipize mataifa jirani mara saba kwa ajili ya matusi waliyokutukana.


jicho kwa jicho, jino kwa jino, mukono kwa mukono, muguu kwa muguu,


Baraka za Yawe ndizo zinazoleta utajiri. Juhudi za mutu haziongezi kitu.


Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.


Mutu mwenye kuwa tayari kusaidia atabarikiwa, maana anagawanya chakula chake na masikini.


Wewe unaonyesha mema yako kwa maelfu ya watu; lakini unawaazibu vilevile watu kwa sababu ya zambi za babu zao. Wewe ni Mungu Mukubwa, mwenye nguvu, Yawe wa majeshi ndilo jina lako.


Na yeyote atakayetoa hata kikombe kimoja tu cha maji ya baridi kwa mumoja wa hao wanaokuwa wadogo kati ya wanafunzi wangu, kwa sababu yeye ni mwanafunzi wangu, kweli ninawaambia: mutu yule hatakosa kupewa zawadi yake.”


Kwa maana mutahukumiwa kufuatana na namna munavyowahukumu wengine, na kipimo kile munachowapimia wengine ndicho kitakachotumiwa kwenu vilevile.


Yesu akawaambia tena: “Muangalie vizuri maneno munayosikia! Mungu atawapimia na kipimo kile munachowapimia wengine, na kuwaongezea hata zaidi.


Mutu akikuomba kitu umupe nacho, na anayekunyanganya vitu vyako, usiombe akurudishie.


Mumupe ndugu masikini kwa moyo safi bila kunungunika, maana kwa ajili ya hayo, Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote na katika kila munalofanya.


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Adoni-Bezeki akasema: “Wafalme makumi saba waliokatwa vidole gumba vya mikono na miguu waliokota makombo chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa kama nilivyotenda.” Wakamupeleka Yerusalema, akakufia kule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ