Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 6:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Ole kwenu ninyi munaoshiba sasa, maana mutasikia njaa. Ole kwenu ninyi munaocheka sasa, maana mutahuzunika na kulia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 6:25
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata akijitukuza katika maisha haya, na kusifiwa kwa sababu ya kufanikiwa,


Huzuni inaweza kufichwa katika kicheko; nyuma ya furaha kunakuja huzuni.


maana nikipata mali mengi nitakusahau; nikisema: “Yawe ni nani?” Au nikiwa masikini nitaiba, na kuzaraulisha jina lako ee Mungu wangu.


Nikasema juu ya kicheko: “Ni wazimu”, na raha: “Iko na faida gani?”


Huzuni ni afazali kuliko kicheko, maana, kwa huzuni ya uso moyo unafurahishwa.


Maana, kicheko cha mupumbafu ni kama mulio wa miiba katika moto. Hayo nayo ni bure.


Lakini kuna wengine waliolewa divai na kuyumbayumba kwa sababu ya pombe kali; makuhani na manabii wamelewa pombe kali, wamevurugika kwa divai. Wanayumbayumba kwa pombe kali; maono yao yamepotoka, wanajikwaa katika kutoa hukumu.


Basi, mimi Yawe ninasema: Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mutasikia njaa; watumishi wangu watakunywa, lakini ninyi mutasikia kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mutafezeheka.


Watu watatangatanga katika inchi, wenye kufazaika sana na wenye njaa. Na wakiwa na njaa, watakasirika na kumulaani mufalme wao vilevile na Mungu wao. Wataangalia juu mbinguni


Manase anashambulia Efuraimu, Efuraimu anashambulia Manase na wote wawili wanashambulia Yuda. Hata hivyo, hasira ya Yawe haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio, na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo. Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni na kunyoa vichwa vyenu upaa, kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee. Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa.


Watateketezwa kama kichaka cha miiba, wao wanaoikalia kulewa. Watateketezwa kama vile majani yenye kukauka.


Lakini Mungu akamwambia: ‘Mupumbafu wewe! Leo leo usiku utakufa. Na sasa, vitu hivi vyote ulivyojitayarishia vitakuwa vya nani?’ ”


Na kule mutalia na kusaga meno, mutakapowaona Abrahamu, Isaka, Yakobo na manabii wote katika Ufalme wa Mungu. Lakini ninyi mutakuwa mumetupwa inje!


Lakini ole kwenu ninyi munaokuwa watajiri, maana hamutapata raha ingine.


Ole kwenu ninyi wakati watu wote watakapowasifu, maana ni hivi babu zao walivyowatendea manabii wa uongo!


Nao wakamuchekelea kwa sababu walijua kwamba amekwisha kufa.


Vilevile kusisikilike maneno ya matusi ya ovyo ovyo wala machafu, kwa maana hayana mafaa. Kinachofaa ni kumushukuru Mungu.


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


Musikitike, mulie na kulalamika. Kucheka kwenu kugeuke kuwa kilio, na furaha yenu igeuke kuwa huzuni.


Wewe unajidai kwamba uko tajiri mwenye mali mengi, wala haukosewi kitu. Lakini haujui kwamba wewe ni mukosefu, mwenye taabu, masikini, kipofu na mwenye kuwa uchi.


Wale ambao zamani walikuwa na chakula tele, sasa wanafanya kazi wapate chakula. Lakini waliokuwa na njaa, sasa hawana njaa tena. Mwanamuke tasa, amezaa watoto saba. Lakini mama mwenye watoto wengi, sasa ameachwa bila mutoto.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ