Hapo Abrahamu akainama uso mpaka chini, akacheka ndani ya moyo wake akiwaza: “Itawezekana kweli mutoto kuzaliwa kwa muzee wa miaka mia moja? Na namna gani, Sara ambaye umri wake ni miaka makumi tisa, ataweza kupata mutoto?”
Juu ya mulima Sayuni, Yawe wa majeshi atawafanyia watu wote karamu ya nyama zenye kunona na divai nzuri, nyama tamu zenye mafuta, pamoja na divai safi.
Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.
Na kama musiponisikiliza, moyo wangu utalia machozi kwenye uficho, kwa sababu ya kiburi chenu. Nitalia kwa uchungu na kutoa machozi, maana watu wa Yawe wanapelekwa katika uhamisho.
Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.
akamwambia hivi: Pita katikati ya Yerusalema, upate kutia kitambulisho kwenye vipaji vya nyuso za watu wanaohuzunika na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika muji huu.
Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”
Nimesumbuka kwa kufanya kazi ngumu, nimepata magumu, nimekesha mara nyingi. Mara nyingi niliteswa na njaa na kiu; mara nyingi nililazimishwa kutokula. Nimeteseka na baridi na ukosefu wa nguo.
Kwa sababu hii ninafurahia uzaifu, matusi, ukosefu, taabu na mateso kwa ajili ya Kristo. Kwa maana wakati ninapokuwa muzaifu, basi ndio wakati ule ninapokuwa na nguvu.
Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.
Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.