Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 6:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Heri kwenu munaokuwa wenye njaa sasa, maana mutashibishwa. Heri kwenu munaolia sasa, maana mutacheka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 6:21
56 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hapo Abrahamu akainama uso mpaka chini, akacheka ndani ya moyo wake akiwaza: “Itawezekana kweli mutoto kuzaliwa kwa muzee wa miaka mia moja? Na namna gani, Sara ambaye umri wake ni miaka makumi tisa, ataweza kupata mutoto?”


Naye Sara akasema: “Mungu amenipatia kicheko; yeyote atakayesikia habari hizi, atacheka pamoja nami.”


Yeye anakunywesha wenye kiu; na anashibisha wenye njaa mazuri.


Macho yangu yanatiririka machozi kama muto, kwa sababu watu hawaishiki sheria yako.


Ninakunyooshea mikono yangu. Ninakuhitaji wewe, kama inchi kavu inavyohitaji mvua.


Lakini mimi nitauona uso wako, maana mimi ni mutu wa haki; nitakapoamuka nitajaa furaha kwa sababu unanitokea.


Yawe ndiye nguvu na ngao yangu; tegemeo la moyo wangu ni kwake. Amenisaidia, nami nikashangilia kwa moyo wote; kwa wimbo wangu ninamushukuru.


Tunapolemewa na makosa yetu, wewe mwenyewe unatusamehe.


Juu ya mulima Sayuni, Yawe wa majeshi atawafanyia watu wote karamu ya nyama zenye kunona na divai nzuri, nyama tamu zenye mafuta, pamoja na divai safi.


Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.


Mushangilie na kufurahi pamoja na Yerusalema, enyi munaoupenda! Mushangilie pamoja nao, enyi wote mulioulilia!


Na kama musiponisikiliza, moyo wangu utalia machozi kwenye uficho, kwa sababu ya kiburi chenu. Nitalia kwa uchungu na kutoa machozi, maana watu wa Yawe wanapelekwa katika uhamisho.


Waliochoka nitawachangamusha, na waregevu nitawapa nguvu.


Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.


Heri ningepata kibanda cha wasafiri katika jangwa, ningewaacha watu wangu na kujiendea. Wote ni wazinzi, ni kundi la watu waasi.


Ikiwa kuna watu walioponyoka, watakimbilia kwenye milima kama njiwa waliotishwa katika bonde. Kila mumoja wao ataomboleza kwa ajili ya zambi zake.


akamwambia hivi: Pita katikati ya Yerusalema, upate kutia kitambulisho kwenye vipaji vya nyuso za watu wanaohuzunika na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika muji huu.


Heri wale wanaokuwa na huzuni, maana Mungu atawafariji!


Heri wale wanaokuwa na njaa na kiu ya kufanya yanayokuwa haki, maana watashibishwa!


Anawatajirisha wenye njaa, lakini amewaacha watajiri mikono mitupu.


Kisha Yesu akawaangalia wanafunzi wake na kusema: “Heri kwenu munaokuwa wamasikini, maana Ufalme wa Mungu ni kwenu.


“Heri ninyi wakati watu wanapowachukia, wanapojitenga nanyi, wanapowatukana na kuchafua jina lenu kwa ajili ya Mwana wa Mutu!


Ole kwenu ninyi munaoshiba sasa, maana mutasikia njaa. Ole kwenu ninyi munaocheka sasa, maana mutahuzunika na kulia.


Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”


Yesu akawaambia: “Mimi ni mukate wa uzima. Anayenikubali hatasikia njaa hata kidogo, na yule anayeniamini hatasikia kiu hata kidogo.


Hata sasa, tunateswa na njaa na kiu, tunakosa nguo, tunapigwa, tunatangatanga bila makao.


Nimesumbuka kwa kufanya kazi ngumu, nimepata magumu, nimekesha mara nyingi. Mara nyingi niliteswa na njaa na kiu; mara nyingi nililazimishwa kutokula. Nimeteseka na baridi na ukosefu wa nguo.


Kwa sababu hii ninafurahia uzaifu, matusi, ukosefu, taabu na mateso kwa ajili ya Kristo. Kwa maana wakati ninapokuwa muzaifu, basi ndio wakati ule ninapokuwa na nguvu.


tunahuzunishwa lakini tunafurahi siku zote. Tunaonekana kama wamasikini lakini tunatajirisha watu wengi, hatuna kitu, lakini tunakuwa na vitu vyote.


Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.


Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.


Nao hawatasikia njaa tena, wala kiu, wala jua halitawapiga tena, wala joto lolote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ