Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 6:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Simoni (Yesu aliyemupa jina la Petro) na ndugu yake Andrea, Yakobo na Yoane, Filipo na Bartolomayo,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 6:14
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na haya ndiyo majina ya hao mitume wake kumi na wawili: kwanza Simoni (anayeitwa vilevile Petro) na ndugu yake Andrea; Yakobo na ndugu yake Yoane, ambao ni wana wa Zebedayo;


kisha Filipo na Bartolomayo, Toma na Matayo aliyekuwa mulipishaji wa kodi; Yakobo mwana wa Alfayo, na Tadeo;


Yesu alipokuwa akitembea pembeni ya ziwa la Galilaya, akawaona wavuvi wawili, waliokuwa wandugu wa tumbo, Simoni (aliyeitwa Petro) na ndugu yake Andrea. Walikuwa wakitupa nyavu katika ziwa.


Yesu alipoendelea mbele kidogo, akawaona wandugu wengine wawili, Yakobo na Yoane, waliokuwa wana wa Zebedayo. Walikuwa ndani ya chombo pamoja na baba yao Zebedayo, wakitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.


Yesu alipoendelea mbele kidogo, akawaona wandugu wengine wawili: Yakobo na Yoane waliokuwa wana wa Zebedayo. Walikuwa ndani ya chombo wakitengeneza nyavu zao.


Yesu na wanafunzi wake walipotoka ndani ya ile nyumba ya kuabudia, mara moja wakaenda kwa nyumba ya Simoni na Andrea, wakiwa pamoja na Yakobo na Yoane.


Kisha akatwaa Petro, Yakobo na Yoane na kwenda nao. Akaanza kuwa na hofu na mahangaiko.


Wale kumi na wawili aliowachagua ni hawa: Simoni (Yesu aliyemupa jina la Petro),


Na Yesu hakuruhusu mutu kumusindikiza, isipokuwa Petro, Yakobo, na Yoane, yule ndugu wa tumbo wa Yakobo.


Nyuma ya siku sita, Yesu aliwatwaa Petro, Yakobo na Yoane, na kuwapeleka kwenye mulima murefu pekee yao. Na kule sura ya Yesu ikageuka mbele yao.


Yakobo na Yoane wana wa Zebedayo waliokuwa wavuvi wenzake na Simoni, walishangaa vilevile. Na Yesu akamwambia Simoni: “Usiogope; tangia sasa utafanya kazi ya kuopoa watu.”


Simoni Petro alipoona mambo hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu na kusema: “Bwana, utoke karibu nami, kwa sababu mimi ni mutu mwenye zambi!”


Kulipokucha, akawaita wanafunzi wake, na kuchagua hawa kumi na wawili katikati yao, akawapanga jina la mitume:


Matayo na Toma, Yakobo mwana wa Alfayo na Simoni (wa kikundi cha Wazeloti),


Kisha Filipo akamukuta Natanaeli, akamwambia: “Tumemwona yule ambaye Musa aliandika habari zake katika kitabu cha Sheria na ambaye manabii walisema juu yake. Ni Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”


Filipo akamwambia: “Bwana, utuonyeshe Baba, na ile itatutoshelea.”


Wakati Yesu alipoinua macho, akaona kundi kubwa la watu wakimufikia. Halafu akamwuliza Filipo: “Wapi tunaweza kununua vyakula kwa kulisha watu hawa?”


Mwanafunzi wake mwingine mumoja anayeitwa Andrea, ndugu ya Simoni Petro, akamwambia:


Walipofika katika muji wakapanda katika chumba cha gorofi walipokuwa wanazoea kukutanana. Na waliokuwa pale ni hawa: Petro, Yoane, Yakobo, Andrea, Filipo, Toma, Bartolomayo, Matayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni wa kikundi cha Wazeloti na Yuda mwana wa Yakobo.


Akaamuru Yakobo, ndugu ya Yoane, auawe kwa upanga.


Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ