Lakini wewe, unapoomba, ingia ndani ya chumba chako, funga mulango na uombe kwa Baba yako asiyeonekana. Na Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.
Yesu akashuka toka kilima pamoja na wanafunzi wake, na kusimama kwenye uwanja. Pale kulikuwa wanafunzi wake pamoja na kundi kubwa sana la watu waliotoka Yerusalema, katika Yudea yote na pande za miji Tiro na Sidona pembeni ya bahari.
Ilipotimia karibu siku nane nyuma ya pale Yesu aliposema maneno hayo, yeye akawatwaa Petro, Yakobo na Yoane, akapanda pamoja nao kwa mulima kwa kuomba.
Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.
“Ninajuta kwamba nimemufanya Saulo kuwa mufalme. Yeye ameacha kunifuata mimi na hajatimiza amri zangu.” Samweli alikasirika, akamulilia Yawe usiku kucha.