Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 6:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Lakini wale wakubwa wakakasirika sana, wakaanza kusemezana wao kwa wao juu ya namna watakavyomutendea Yesu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 6:11
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa.


Wanafunzi wakaanza kusemezana hivi wao kwa wao: “Anasema hivi kwa sababu hatuna mikate.”


Wakubwa wa makuhani na Wafarisayo waliposikia mifano hiyo Yesu aliyoitumia, wakatambua kwamba alisema juu yao.


Watu wote waliokuwa ndani ya ile nyumba ya kuabudia, wakakasirika sana wakati waliposikia maneno hayo.


Yesu akawaangalia wote waliokuwa pale, kisha akamwambia yule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Naye akafanya vile, na mukono wake ukakuwa muzima tena.


Katika siku zile, Yesu akapanda juu ya kilima kwenda kuomba na kukesha usiku wote akiomba Mungu.


Basi wakubwa wa makuhani na Wafarisayo wakakusanya Baraza yao Kubwa, na kusema: “Tufanye nini kwa kuona mutu huyu anaonyesha vitambulisho vingi?


Kisha mambo hayo, Yesu akatembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea katika Yudea, kwa sababu Wayuda walitaka kumwua.


Mara nyingi niliwaazibu katika nyumba za kuabudia na kuwashurutisha wakane imani yao. Niliwakasirikia kupita kipimo, hata nikaenda kuwatesa katika miji ya inchi za kigeni.


Basi wakawaamuru watoke katika Baraza Kubwa na kwenda inje, nao wakaulizana shauri wao kwa wao,


Lakini Petro na Yoane wakawajibu: “Muamue ninyi wenyewe, ni haki mbele ya Mungu kuwatii ninyi kuliko kumutii Mungu?


Wajumbe wa lile Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kutaka kuwaua mitume.


Wajumbe wa Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kumusagia Stefano meno.


Lakini hawataendelea mbali sana, kwa sababu upumbafu wao utaonekana wazi mbele ya watu wote, sawa ilivyokuwa kwa Yane na Yambure.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ