Yule mwanamuke akamwambia Elia: “Ewe mutu wa Mungu, kuna maneno gani kati yako nami? Kumbe ulikuja kwangu kwa kuzifichua zambi zangu na kusababisha kifo cha mwana wangu?”
Basi, mimi nikasema: Ole kwangu! Mimi nimeangamia, maana, midomo yangu ni michafu, na watu ninaoishi nao ni wenye midomo michafu. Hata hivyo, kwa macho yangu mwenyewe, nimemwona Mufalme, Yawe wa majeshi.
Wakaingia ndani ya nyumba, wakamwona mutoto pamoja na mama yake, Maria. Wakapiga magoti na kumwabudu mutoto. Kisha wakafungua mizigo yao na kumutolea zawadi ya zahabu, ubani na marasi.
Halafu wakawafanyia wale wenzao waliokuwa ndani ya chombo kingine alama kwa mikono, kusudi wakuje kuwasaidia. Wakakuja, wakajaza vyombo vyote viwili na samaki wengi, hata vyombo vikaanza kuzama.
Kwa maana wakati wa sasa tunaona kama mwenye kuangalia ndani ya kioo kisichoonyesha wazi, lakini wakati utakaokuja tutaona waziwazi. Kwa sasa ninajua tu mambo machache, lakini nyuma nitajua kwa utimilifu kama vile Mungu anavyonijua mimi.
Wakati nilipomwona, nikaanguka chini kwa rafla mbele yake kama vile mufu. Lakini akaweka mukono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
Kisha, wakaaji wa muji wa Beti-Semesi wakasema: “Nani anayeweza kusimama mbele ya Yawe, huyu Mungu mutakatifu? Atakwenda kwa nani kusudi aondoke kwetu?”