Wavuvi watasimama kandokando ya bahari, na nafasi toka Engedi mpaka Eni-Eglaimu itakuwa ya kuanikia nyavu. Kutakuwa aina nyingi za samaki kama zinavyokuwa katika bahari ya Mediteranea.
Basi wanafunzi wake wakamujongelea, wakamwamusha wakisema: “Bwana, Bwana, tunakufa!” Yesu alipoamuka, akakaripia zoruba, nayo ikakoma na maji yakatulia.
Watu wale walipokuwa wakiachana na Yesu, Petro akamwambia: “Bwana, ni vizuri kuona sisi tuko hapa. Tujenge vibanda vitatu, kimoja chako, kimoja cha Musa na kingine cha Elia.” (Naye alisema hayo bila kufikiri.)
Simoni Petro akawaambia wenzake hivi: “Ninakwenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia: “Na sisi vilevile tutakwenda pamoja nawe.” Basi wakaondoka, wakaingia katika chombo. Usiku ule hawakupata kitu.