Kisha majuma hayo makumi saba na mawili, yule aliyepakwa mafuta atauawa na hatabaki na kitu. Muji na Pahali Patakatifu Sana vitaharibishwa na waaskari wa mutawala atakayekuja kushambulia. Mwisho wake utafika kama mafuriko, kukiwa vita na maangamizi kama yalivyopangwa na Mungu.
Yesu akawajibu: “Munafikiri kwamba warafiki za bwana-arusi wanaweza kufanya kilio wakati bwana-arusi angali pamoja nao? Hapana! Lakini kutakuwa siku bwana-arusi atakapoondoshwa kati yao; ni siku zile watafunga kula.
Yesu akawaambia mufano huu vilevile: “Hakuna mutu anayekata kiraka kwenye nguo mupya na kukishonea juu ya nguo ya zamani. Kama anafanya vile, atakuwa amepasua ile nguo mupya na kile kiraka cha nguo mupya hakitashikamana na nguo ya zamani.
Watoto wangu, ningali pamoja nanyi kwa muda mufupi tu. Mutanitafuta, lakini sawasawa nilivyowaambia Wayuda, ninawaambia ninyi vilevile kwamba hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.
Yeye anapaswa kubaki mbinguni mpaka zitakapotimia zile nyakati Mungu atakapotengeneza vitu vyote sawa vile alivyosema tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake watakatifu.
Musinyimane, isipokuwa tu mumepatana na kwa muda tu kusudi mupate wakati wa kujitoa kwa kufunga na kuomba. Kisha munaweza kurudiliana tena kusudi Shetani asiwajaribu katika uzaifu wenu.
Nimesumbuka kwa kufanya kazi ngumu, nimepata magumu, nimekesha mara nyingi. Mara nyingi niliteswa na njaa na kiu; mara nyingi nililazimishwa kutokula. Nimeteseka na baridi na ukosefu wa nguo.