Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 5:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Yakobo na Yoane wana wa Zebedayo waliokuwa wavuvi wenzake na Simoni, walishangaa vilevile. Na Yesu akamwambia Simoni: “Usiogope; tangia sasa utafanya kazi ya kuopoa watu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 5:10
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Ufalme wa mbinguni unafanana vilevile na wavuvi wamoja waliotupa wavu ndani ya ziwa, nao ukakusanya samaki wa kila namna.


Lakini mara moja Yesu akasema nao, akiwaambia: “Mujipe moyo, ni mimi! Musiogope!”


Wana wa Zebedayo pamoja na mama yao wakamufikia Yesu. Yule mama akapiga magoti mbele yake, kwa kumwomba kitu kimoja.


Yesu akawaambia: “Munifuate, nami nitawaweka kwa kazi ya kuopoa watu.”


Yesu alipoendelea mbele kidogo, akawaona wandugu wengine wawili, Yakobo na Yoane, waliokuwa wana wa Zebedayo. Walikuwa ndani ya chombo pamoja na baba yao Zebedayo, wakitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.


Yesu akawaambia: “Munifuate, nami nitawaweka kwa kazi ya kuopoa watu.”


Halafu wakawafanyia wale wenzao waliokuwa ndani ya chombo kingine alama kwa mikono, kusudi wakuje kuwasaidia. Wakakuja, wakajaza vyombo vyote viwili na samaki wengi, hata vyombo vikaanza kuzama.


Simoni na wote waliokuwa pamoja naye walishangaa sana kwa sababu ya wingi wa samaki waliowapata.


Simoni (Yesu aliyemupa jina la Petro) na ndugu yake Andrea, Yakobo na Yoane, Filipo na Bartolomayo,


Simoni Petro, Toma (anayeitwa Pacha), Natanaeli (wa muji Kana katika Galilaya), nao wana wa Zebedayo pamoja na wanafunzi wengine wawili wa Yesu, wote walikuwa pamoja.


Wote wakapewa Roho Mutakatifu na kuanza kusema kwa luga mbalimbali kwa kadiri Roho alivyowawezesha kusema.


Kwa ngambo ya Tito, yeye ni mwenzangu, ninafanya kazi pamoja naye kwa ajili yenu. Nao wale wandugu wengine wanaomusindikiza, ni wajumbe wa makanisa wanaotumika kwa ajili ya utukufu wa Kristo.


Kwa njia hiyo wanaweza tena kupata ufahamu na kuponyoka katika mitego ya Shetani, aliyewanasa na kuwafanya watimize mapenzi yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ