Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 4:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Yesu akamukaripia, akimwamuru hivi: “Nyamaza, na utoke ndani ya mutu huyu!” Na yule pepo akamutupa yule mutu chini mbele ya watu, na kutoka ndani yake pasipo kumwumiza.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 4:35
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Mungu anamwambia mutu mwovu: “Kwa nini kutajataja tu masharti yangu? Kwa nini unasemasema juu ya agano langu?


Malaika wa Yawe akamwambia yule Shetani: Yawe akulaani, ewe Shetani! Kweli, Yawe aliyechagua Yerusalema akulaani! Huyu ni kama kipande cha kuni kilichoopolewa ndani ya moto!


Yesu akamukaripia yule pepo aliyekuwa ndani ya yule mutoto, naye akamwacha, na tangia saa ile ile yule mutoto akapona.


Yesu akawajibu: “Sababu gani munaogopa kama hivi? Hakika imani yenu ni ndogo!” Halafu akasimama, akakaripia zoruba na maji na kukakuwa kimya kabisa ndani ya ziwa.


Yule pepo akamutikisa mutu yule kwa nguvu, akatoka ndani yake, akilalamika kwa nguvu.


Yesu akaamuka, akakaripia ile zoruba na kuiambia ziwa: “Kimya! Tulizana!” Basi zoruba ikakoma na kukakuwa kimya kabisa.


Yule pepo akalalamika, akamutikisatikisa mutoto kwa nguvu na kutoka ndani yake. Mutoto akaonekana sawa amekufa, hata watu wengi wakaanza kusema kwamba amekufa.


Lakini mutu mwingine mwenye nguvu zaidi akimushambulia na kumushinda, anamunyanganya silaha zake alizotegemea na kugawanya vitu vya unyanganyi anavyokuwa navyo.


Yesu akawaambia: “Hakika mutaniambia fumbo hili: ‘Muganga, ujiponyeshe wewe mwenyewe!’ Na vilevile mutaniambia hivi: ‘Tumesikia mambo yote uliyotenda katika muji Kapernaumu, basi uyafanye hapa vilevile katika muji wako.’ ”


Basi akainama kunapokuwa yule mama, akaamuru ile homa itoke ndani yake, naye akapona. Na mara moja akasimama na kuanza kuwashugulikia.


Pepo wakatoka ndani ya watu wengi, wakilalamika, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakaripia, na hakuwaachilia waseme neno, kwa sababu walijua kwamba yeye ndiye Kristo.


Basi wanafunzi wake wakamujongelea, wakamwamusha wakisema: “Bwana, Bwana, tunakufa!” Yesu alipoamuka, akakaripia zoruba, nayo ikakoma na maji yakatulia.


Pepo anapomukamata, mara moja mutoto analalamika, na yule pepo anamutikisatikisa kwa nguvu hata pofu inamutoka. Huyo pepo hatoki ndani yake upesi, naye anamutesa sana.


Yule mutoto alipokuwa akijongea karibu na Yesu, yule pepo akamutupa chini na kumutikisa kwa nguvu. Lakini Yesu akamukaripia yule pepo na kumuponyesha mutoto. Kisha akamurudisha kwa baba yake.


Kwa sababu hii, ninyi munaokaa mbinguni, nayo mbingu kwa jumla, mushangilie! Ole kwenu ninyi munaokaa katika dunia na katika bahari kwa maana yule Mwovu ameshuka kwenu, naye anajaa na hasira, kwa sababu anajua kwamba wakati unaomubakilia ni mudogo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ