29 Wakasimama, wakamusukuma Yesu hata inje ya muji wao, uliojengwa juu ya kilima. Wakamupeleka kwenye maporomoko kusudi wamutupe chini.
Na wengine watu elfu kumi, wakakamatwa na kuwapandisha juu ya jiwe kubwa na kuwatupa chini toka juu ya jiwe, wakavunjika vipandevipande.
Waovu wanachomoa panga na kuvuta pinde zao, wapate kuwaua wamasikini na wakosefu; wawachinje watu wenye mwenendo sawa.
Halafu Yawe akamwambia Musa: Mutu huyo anapaswa kuuawa; Waisraeli wote pamoja watamupiga mawe inje ya kambi.
Watu wote waliokuwa ndani ya ile nyumba ya kuabudia, wakakasirika sana wakati waliposikia maneno hayo.
Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Abrahamu. Lakini munatafuta kuniua, kwa sababu munakataa kukubali mafundisho yangu.
Lakini sasa munatafuta kuniua ijapokuwa nimewaambia ukweli niliousikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya vile.
Kwa ajili ya hii, wakaokota mawe kwa kumutupia. Lakini Yesu akajificha na kutoka ndani ya hekalu.
Kwa sababu hii Yesu vilevile aliuawa mbali na muji kusudi awatakase watu wake kwa njia ya damu yake mwenyewe.