Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 4:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Watu wote waliokuwa ndani ya ile nyumba ya kuabudia, wakakasirika sana wakati waliposikia maneno hayo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 4:28
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, Asa akamukasirikia sana nabii Hanani, hata akamuweka katika kifungo; maana amekuwa na hasira kubwa naye juu ya maneno yale. Wakati uleule, Asa akaanza kuwatesa vikali wamoja kati ya watu.


Basi, wakamutwaa Yeremia wakamutia katika kisima cha Malkia mwana wa mufalme ambacho kilikuwa katika kiwanja cha walinzi. Walimushusha Yeremia ndani kwa kamba. Ndani ya kisima hicho hamukukuwa maji lakini matope, naye Yeremia akazama katika matope.


Herode alipoona kwamba wale watu wenye elimu wamemudanganya, akakasirika sana. Akatuma watu Betelehemu na popote kandokando yake kwa kuua watoto wote waliokuwa na umri wa miaka miwili na chini yake. Alifanya vile kufuatana na jinsi alivyohakikishwa na wale wenye elimu juu ya wakati nyota ilipotokea.


Vilevile kulikuwa watu wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna mumoja kati yao aliyetakaswa, isipokuwa tu Namani wa inchi ya Suria.”


Wakasimama, wakamusukuma Yesu hata inje ya muji wao, uliojengwa juu ya kilima. Wakamupeleka kwenye maporomoko kusudi wamutupe chini.


Lakini wale wakubwa wakakasirika sana, wakaanza kusemezana wao kwa wao juu ya namna watakavyomutendea Yesu.


Wajumbe wa lile Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kutaka kuwaua mitume.


Wajumbe wa Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kumusagia Stefano meno.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ