Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 4:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Nao wote wakamufurahia na kushangaa na maneno mazuri aliyosema. Wakasema: “Huyu si mwana wa Yosefu?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 4:22
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Moyo wangu umejaa mawazo mazuri: ninamutungia mufalme mashairi yangu, ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi hodari.


Ujifungie upanga wako, ewe shujaa! Wewe ni mutukufu na mwenye mamlaka.


Midomo ya wenye haki inajua mambo yatakayokubaliwa, lakini vinywa vya waovu vinasema tu maovu.


Mwenye hekima ndani ya moyo anaitwa mwenye akili; neno la kupendeza linawavuta watu.


Neno linalosemwa kwa wakati unaofaa, ni kama michoro ya zahabu juu ya feza.


Maneno ya mwenye hekima yanamupa upendeleo; lakini maneno ya mupumbafu yanamwangamiza.


Kinywa chake kinajaa maneno matamu. Yeye wote anapendeza. Basi, hivi ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa, ndivyo rafiki yangu anavyokuwa, enyi wabinti wa Yerusalema.


Bwana wetu Yawe amenifundisha jinsi ya kusema, kusudi niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubui ananipa hamu ya kusikiliza mambo anayotaka kunifundisha.


Na wote waliomusikia walishangaa kuona akili yake na majibu yake.


Wazazi wake walipomwona, wakashangaa sana. Mama yake akamwuliza: “Mutoto wangu, kwa nini umetufanyia kama hivi? Mimi na baba yako tulikutafuta tukiwa na wasiwasi.”


Kwa maana mimi mwenyewe nitawapa masemi na hekima hata waadui zenu hawataweza kuyapinga wala kuyakataa.


Halafu akaanza kuwaambia: “Maandiko haya yametimia leo.”


Kisha Filipo akamukuta Natanaeli, akamwambia: “Tumemwona yule ambaye Musa aliandika habari zake katika kitabu cha Sheria na ambaye manabii walisema juu yake. Ni Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”


Nao wakasema: “Huyu si Yesu mwana wa Yosefu? Si tunawajua baba yake na mama yake? Namna gani anaweza kusema sasa kwamba alishuka toka mbinguni?”


Walinzi wakajibu: “Hatujasikia mutu akisema sawasawa na mutu yule!”


lakini hawakuweza kumushinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya Roho Mutakatifu aliyemwongoza kusema.


Ufundishe maneno ya kweli watu wasiyoweza kubishia, hata wale wanaokupinga wapate haya kwa kukosewa na neno baya la kusema juu yetu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ