Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kule akajaribiwa na Shetani kwa muda wa siku makumi ine. Kwa muda ule, yeye hakukula kitu. Na wakati siku zile zilipotimia, akasikia njaa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 4:2
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


Elia akaamuka, akakula na kunywa. Kisha akatembea kwa nguvu ya chakula hicho mwendo wa siku makumi ine, muchana na usiku, mpaka Horebu kwenye mulima wa Mungu.


“Kwenda uwakusanye pamoja Wayuda wote wanaokuwa katika muji wa Susani. Mufunge, musikule wala musikunywe kwa siku tatu, usiku na muchana, kwa ajili yangu. Na mimi na wajakazi wangu tutafanya vile vile. Kisha, nitamwendea mufalme, ingawa ni kinyume cha sheria. Kama ni kuuawa, niuawe.”


Musa akaingia ndani ya lile wingu, akapanda kwenye mulima. Alikaa kule kwa muda wa siku makumi ine, muchana na usiku.


Musa alikaa kule kwenye mulima pamoja na Yawe siku makumi ine, muchana na usiku. Hakukula chakula wala kunywa maji. Aliandika maneno yote ya agano na zile amri kumi.


Kisha mufalme akawatangazia wakaaji wa Ninawe: Mimi mufalme, pamoja na wakubwa wangu, ninatoa amri hii: Kusikuwe mutu yeyote, ngombe au nyama yeyote wa kufugwa, atakayeonja kitu chochote. Hairuhusiwi kwa mutu yeyote au nyama kula au kunywa.


Kesho yake asubui, Yesu alipokuwa akirudia Yerusalema, akasikia njaa.


Naye Yesu alipomaliza kufunga kula chakula kwa muda wa siku makumi ine, muchana na usiku, akasikia njaa.


Halafu Shetani akamufikia na kumwambia: “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili ligeuke mukate.”


Pale kulikuwa kisima kilichokuwa cha Yakobo. Yesu akaikaa kwa ukingo wa kisima, kwa sababu alikuwa amechoka na safari. Ilikuwa karibu na saa sita za muchana.


Kisha nikalala uso mpaka chini mbele ya Yawe, kama vile mbele, kwa muda wa siku makumi ine usiku na muchana. Sikukula chakula wala kunywa maji, kwa sababu ya zambi muliyokuwa mumetenda kwa kufanya maovu mbele ya Yawe kwa kumukasirikisha.


“Kwa hiyo, nikalala uso mpaka chini mbele ya Yawe siku hizo makumi ine, usiku na muchana, kwa sababu Yawe alikuwa amesema atawaangamiza.


Nilipopanda juu ya mulima kupokea vibao vya mawe ambavyo kuliandikwa agano ambalo Yawe alifanya nanyi, nilikaa huko siku makumi ine, usiku na muchana; sikukula wala kunywa chochote.


Na kwa sababu yeye mwenyewe alijaribiwa na kuteswa, anaweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Kwa muda wa siku makumi ine, asubui na magaribi, yule Mufilistini Goliati alijitokeza, akasimama na kuwazarau waaskari wa Waisraeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ