Elia akaamuka, akakula na kunywa. Kisha akatembea kwa nguvu ya chakula hicho mwendo wa siku makumi ine, muchana na usiku, mpaka Horebu kwenye mulima wa Mungu.
“Kwenda uwakusanye pamoja Wayuda wote wanaokuwa katika muji wa Susani. Mufunge, musikule wala musikunywe kwa siku tatu, usiku na muchana, kwa ajili yangu. Na mimi na wajakazi wangu tutafanya vile vile. Kisha, nitamwendea mufalme, ingawa ni kinyume cha sheria. Kama ni kuuawa, niuawe.”
Musa alikaa kule kwenye mulima pamoja na Yawe siku makumi ine, muchana na usiku. Hakukula chakula wala kunywa maji. Aliandika maneno yote ya agano na zile amri kumi.
Kisha mufalme akawatangazia wakaaji wa Ninawe: Mimi mufalme, pamoja na wakubwa wangu, ninatoa amri hii: Kusikuwe mutu yeyote, ngombe au nyama yeyote wa kufugwa, atakayeonja kitu chochote. Hairuhusiwi kwa mutu yeyote au nyama kula au kunywa.
Pale kulikuwa kisima kilichokuwa cha Yakobo. Yesu akaikaa kwa ukingo wa kisima, kwa sababu alikuwa amechoka na safari. Ilikuwa karibu na saa sita za muchana.
Kisha nikalala uso mpaka chini mbele ya Yawe, kama vile mbele, kwa muda wa siku makumi ine usiku na muchana. Sikukula chakula wala kunywa maji, kwa sababu ya zambi muliyokuwa mumetenda kwa kufanya maovu mbele ya Yawe kwa kumukasirikisha.
Nilipopanda juu ya mulima kupokea vibao vya mawe ambavyo kuliandikwa agano ambalo Yawe alifanya nanyi, nilikaa huko siku makumi ine, usiku na muchana; sikukula wala kunywa chochote.
Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.