Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yesu, akarudia toka kwenye muto Yordani, akijazwa na Roho, na Roho huyo akamwongoza kwenda katika jangwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 4:1
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninaogopa kwamba mara tu nitakapoondoka, Roho wa Yawe atakunyanyua na kukupeleka pahali nisipopajua! Nikienda kumwambia Ahabu kwamba uko hapa, naye akikutafuta na asikupate, ataniua mimi, ingawa mimi mutumishi wako ninamwogopa Yawe tangu ujana wangu.


naye akatembea mwendo wa siku nzima kuingia katika jangwa. Basi, akafika, akaikaa chini ya muti mumoja wa muretemu. Halafu, akaomba apate kufa, akisema: “Inatosha! Siwezi tena. Ee Yawe, sasa utoe uzima wangu. Mimi si bora kuliko babu zangu.”


Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


Basi, Roho akaninyanyua juu na kunipeleka mbali. Yawe alinijaza uwezo wake. Nami nikaenda nikiwa na uchungu na hasira katika roho yangu.


Yesu alipokwisha kubatizwa na kutoka ndani ya maji, mara moja mbingu zikafunguka, naye akamwona Roho wa Mungu akishuka kwa mufano wa njiwa na kukaa juu yake.


Na ilimutokea Simeoni kuingia ndani ya hekalu, akiongozwa na Roho. Wazazi walipomuleta mutoto wao Yesu kusudi wamutendee sawa ilivyoagizwa na Sheria,


Basi Yoane akapita katika inchi zote zinazokuwa pembeni ya muto Yordani, akihubiri. Akawaambia watu wageuke toka zambi zao, wabatizwe, na Mungu atawaondolea zambi.


Yesu akarudia Galilaya akijazwa na uwezo wa Roho, na habari zake zikaenea fasi zote katika pande zile.


“Roho wa Bwana yuko pamoja nami, maana amenichagua niwahubirie wamasikini Habari Njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kwamba watakombolewa nao vipofu kwamba wataona. Amenituma kuwapa wanaoteswa uhuru,


Yoane akatoa ushuhuda huu: “Nimemwona Roho akishuka juu yake toka mbinguni kwa mufano wa njiwa na kukaa juu yake.


Aliyetumwa na Mungu anasema maneno ya Mungu, kwa sababu Mungu anamujaza Roho wake kwa uwingi.


mpaka siku ile aliponyanyuliwa mbinguni. Mbele ya kunyanyuliwa kule, alitoa maagizo kwa njia ya Roho Mutakatifu kwa watu aliokuwa amewachagua kuwa mitume wake.


Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.


Walipotoka ndani ya maji, kwa rafla Roho wa Bwana akamutowesha Filipo, na yule mukubwa hakumwona tena, lakini akaongeza safari yake katika furaha.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ