Yesu aliposikia maneno haya, akamwambia: “Ungali unakosewa na kitu kimoja tu: uuzishe vitu vyote unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudie unifuate!”
Lakini Zakayo akasimama mbele ya Bwana na kumwambia: “Bwana! Ninawapa masikini nusu ya mali zangu, na kama nimetwaa kitu cha mutu kwa kumudanganya, nitamurudishia mara ine sawa na kitu kile.”
Wamoja walizani kama Yesu amemwambia aende kununua vitu walivyohitaji kwa sikukuu, au aende kuwasaidia wamasikini, kwa sababu Yuda ndiye aliyekuwa akichunga mufuko wa feza.)
Yeye alikuwa mwenye kuogopa Mungu, naye alimwabudu Mungu pamoja na watu wote waliokuwa kwake. Aliwasaidia wamasikini wengi, naye alikuwa akimwomba Mungu siku zote.
Kornelio akamukazia macho akiwa ameshikwa na woga, akamwuliza: “Bwana, ni nini?” Malaika akamujibu: “Mungu amesikia maombi yako na kupendezwa na misaada unayotoa kwa wamasikini, na kwa hiyo anakukumbuka.
Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.
Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.
Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.
Mutu akiwa na mali ya dunia hii naye akimwona ndugu yake katika hitaji, lakini hataki kumusikilia huruma, mutu yule anaweza kusema kwamba anamupenda Mungu?
Kama mutu akisema “Ninamupenda Mungu,” naye anamuchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana yule asiyemupenda ndugu yake anayemwona, hawezi kumupenda Mungu asiyemwona.