Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.
Tangia wakati ule Yesu akaanza kuwaambia wanafunzi wake waziwazi kwamba ni sherti kwake kwenda Yerusalema, ateswe kule na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria, auawe, na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.
Lakini kijana yule akawaambia: “Musishituke! Munamutafuta Yesu wa Nazareti aliyetundikwa juu ya musalaba. Yeye amefufuka, hayuko hapa. Muangalie, hapa ni pahali walipomuweka.
Kisha Yesu akaanza kuwafundisha wanafunzi wake, akisema: “Sherti Mwana wa Mutu ateswe na kukataliwa na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani pamoja na walimu wa Sheria. Atauawa na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake atafufuka.”
Kwa sababu ya woga, wale wanawake wakainama uso mpaka chini. Lakini wale watu wakawaambia: “Kwa sababu gani munamutafuta yule anayekuwa muzima kati ya waliokufa?
Naye akaongeza kuwaambia: “Sherti Mwana wa Mutu ateswe na kukataliwa na wasimamizi wa watu, pamoja na walimu wa Sheria. Atauawa na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”