Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 24:47 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

47 Iliandikwa vilevile kwamba kwa jina lake watahubiri mataifa yote, kuanzia Yerusalema, kusudi wageuke toka katika zambi na wapate kusamehewa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 24:47
52 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anayekubariki, nitamubariki, anayekulaani, nitamulaani. Kwa njia yako, nitabariki mataifa yote ya dunia.”


Wamasikini watakula na kushiba; wanaomutafuta Yawe watamusifu. Mungu awajalie waishi milele!


Inchi imetoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu, ametubariki.


Mataifa yote uliyoumba, yatakuja kukuabudu, ee Bwana; yatatangaza ukubwa wa jina lako.


Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitasimika bendera kwa kuita mataifa; nitayaonyesha kitambulisho. Nayo yatawarudishia wana wenu wakiwabeba kwenye kifua, vilevile na wabinti zenu kwenye mabega.


Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.


Ni kitu gani nilichokosa kulifanyia shamba langu? Nilipotazamia lizae zabibu nzuri, mbona basi, likazaa zabibu chungu?


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Lakini sasa ameyashangaza mataifa mengi. Wafalme watapumbazika kwa sababu yake, maana wataona mambo ambayo hawajapata kuambiwa, na kufahamu mambo ambayo hawajapata kusikia.


Wala hawatafundishana tena kila mutu na jirani yake, na kila mutu na ndugu yake na kusema “Mumujue Yawe”, kwa sababu wote, wadogo kama vile wakubwa, watanijua mimi Mungu. Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena zambi zao.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.


Siku hiyo, nitajibu kwa mahitaji ya mbingu ya kunyesha mvua, mbingu nazo zitajibu kwa mahitaji ya udongo. –Ni ujumbe wa Yawe.–


mataifa mengi yataufikia na kusema: Tuende juu kwenye mulima wa Yawe, tuende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo, kusudi atufundishe njia zake, nasi tuzifuate. Maana sheria itatoka kule Sayuni; na neno la Yawe kule Yerusalema.


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Basi muwaendee watu wa mataifa yote kusudi wapate kuwa wanafunzi wangu, mukiwabatiza kwa jina la Baba, la Mwana na la Roho Mutakatifu.


akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”


Muende kujifunza maana ya Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu.’ Kwa maana sikukuja kuwaita wenye haki kunifuata, lakini watenda mabaya.”


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema, wewe unayewaua manabii na wajumbe ambao Mungu anakutumia kwa kuwatupia mawe. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Manabii wote wanamushuhudia Yesu kwamba kila mutu anayemwamini atasamehewa zambi zake kwa uwezo wa jina lake.”


Wandugu waamini waliposikia maneno hayo, wakatulia na kumusifu Mungu, wakisema: “Kumbe Mungu amewajalia hata watu wa mataifa mengine vilevile kusudi waweze kugeuka toka zambi na kupata uzima kamili.”


Halafu Paulo na Barnaba wakawaambia bila woga: “Ilitupasa kwanza kuhubiri Neno la Mungu kwenu. Lakini kwa kuona mumelikataa na kujihesabu ninyi wenyewe kwamba uzima wa milele haufai kwenu, basi tunashugulika na watu wa mataifa mengine.


Petro akawajibu: “Mugeuke toka katika zambi zenu, na kila mumoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo, na Mungu atawasamehe zambi zenu. Hivi mutapokea zawadi ya Roho Mutakatifu.


Nimewaonya Wayuda wa mataifa mengine kwamba wanapaswa kumugeukia Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Lakini kwanza nilihubiri wakaaji wa Damasiki, na wa Yerusalema na wa jimbo lote la Yudea nao watu wa mataifa mengine vilevile. Nilihubiri kwao kwamba wageuke toka zambi zao na kumurudilia Mungu, nao waonyeshe kwa njia ya matendo yao kwamba wamegeuka.


“Na kwa kumaliza, basi mujue kwamba habari ya wokovu huu wa Mungu imetumwa kutangazwa kwa watu wa mataifa mengine, nao wataisikia!” [


Basi mugeuke toka katika zambi, mumurudilie Mungu, kusudi awasamehe zambi zenu.


“Hivi hakuna anayeweza kuokolewa kwa njia ya mutu mwingine yeyote, kwa maana katika dunia nzima hakuna jina lingine lolote watu walilopewa lenye uwezo wa kuwaokoa.”


Mungu alimupa utukufu na kumwikalisha na mamlaka karibu naye na kumuweka kuwa Mutawala na Mwokozi. Na hivi Waisraeli wataweza kugeuka toka zambi zao na Mungu atawasamehe.


Sheria ilitokea na kusababisha kuongezeka kwa makosa, lakini nafasi yoyote palipozidi zambi, neema ilizidi sana.


Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


Kwa maana Mungu alitaka kuwafunulia watu hao siri ya mupango wake wenye utajiri mukubwa alioufanya kwa ajili ya mataifa yote. Nayo siri ile ni kwamba Kristo ni ndani yenu, naye ndiye anayetuletea tumaini kwamba tutashiriki katika utukufu wa Mungu.


Ninawaandikia ninyi watoto wangu, kwa sababu mumesamehewa zambi zenu kwa jina la Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ