Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 24:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Alipokuwa akiikaa kula chakula pamoja nao, akatwaa mukate na kuubariki. Kisha akaumega na kuwapatia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 24:30
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha kuwaamuru watu waikae juu ya majani, Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Akamega ile mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakaigawanya kwa kundi la watu.


Kisha akatwaa ile mikate saba na zile samaki, akamushukuru Mungu, akaimega na kuwapa wanafunzi wake wavigawanye kwa watu.


Walipokuwa wakikula, Yesu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema: “Mutwae na mukule, huu ni mwili wangu.”


Walipokuwa wakikula, akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema: “Mutwae, huu ni mwili wangu.”


Kisha Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Akamega ile mikate, akawapa wanafunzi wake pamoja na zile samaki mbili kusudi waigawanyie watu wote.


Basi Yesu akawaamuru watu waikae chini. Kisha akakamata ile mikate saba, akamushukuru Mungu, akaimega na kuwapa wanafunzi wake waigawanye kwa watu; nao wanafunzi wakaigawanya.


Halafu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa akisema: “Huu ni mwili wangu [unaotolewa kwa ajili yenu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka.”


Lakini wakamusihi sana abakie pamoja nao, kwa maana ilikuwa magaribi na giza lilitaka kuingia. Basi akaingia ndani ya nyumba kubakia pamoja nao.


Nao vilevile wakawaelezea mambo yote yaliyotokea katika njia na namna walivyomutambua Yesu wakati alipomega mukate.


Kisha Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Halafu akaimega, akawapa wanafunzi waigawanyie watu.


Kisha Yesu akatwaa ile mikate, akamushukuru Mungu na kuigawanya kwa watu walioikaa pale. Akawapa samaki vilevile kwa kadiri walivyotaka.


Nao walikuwa wakijitoa kufuata mafundisho ya mitume, kuishi katika ushirika wa kindugu, kumega mukate na kuomba.


Kila siku walikuwa wakikusanyika pamoja katika hekalu, nao walikula chakula pamoja katika nyumba zao kwa furaha na katika unyenyekevu.


Kisha kusema maneno hayo, Paulo akatwaa mukate, akamushukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, na akaanza kula.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ