44-45 Ilikuwa karibu na saa sita ya muchana, jua likafifia, kukakuwa giza katika inchi yote mpaka saa tisa. Pazia la hekalu likapasuka katikati.
Mungu akaleta giza juu ya inchi; lakini Wamisri wakakataa kutii amri zake.
Ole kwenu ninyi munaoingojea kwa hamu siku ya Yawe! Kwa nini munaitaka sana siku hiyo? Siku hiyo, itakuwa siku ya giza na si ya mwangaza!
Siku hiyo, nitalifanya jua litue pa saa sita za muchana, na kuijaza inchi giza wakati wa muchana. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Tangia saa sita ya muchana, giza lilikuwa katika inchi yote mpaka saa tisa.
makaburi yakafunguka, na watakatifu wengi waliokufa zamani wakafufuliwa.
Mukubwa wa waaskari aliyekuwa akisimama mbele ya Yesu, alipoona namna alivyokata roho, akasema: “Hakika mutu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
Siku ile ilikuwa siku ya matayarisho ya Pasaka, karibu na saa sita. Pilato akawaambia Wayuda: “Mufalme wenu huyu!”
Jua litatiwa giza, mwezi utakuwa kama damu, mbele ya kutimia kwa siku ya Bwana, ile siku kubwa na ya utukufu.