Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 23:43 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

43 Yesu akamujibu: “Kweli ninakuambia wewe: leo hii utakuwa pamoja nami katika Paradizo.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 23:43
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha niliitikia makosa yangu mbele yako, wala sikuficha uovu wangu. Nilisema kwamba nitaungama makosa yangu mbele ya Yawe. Nawe ukanisamehe zambi yangu.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.


Hata mbele hawajaniita, mimi nitawaitikia; mbele hawajamaliza kusema, nitakuwa nimewajibu.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Kwa maana Mwana wa Mutu alikuja kutafuta na kuokoa yule aliyepotea.”


Na akaongeza kusema: “Ee Yesu, usinisahau wakati utakapokuja katika ufalme wako!”


Nami nitakapokwisha kuwatayarishia ninyi nafasi, nitarudi tena na kuja kuwatwaa, kusudi pahali nitakapokuwa, ninyi mupate kuwa pale vilevile.


“Baba, ninataka wale ulionipa wakuwe pamoja nami pahali nitakapokuwa, nao waone utukufu wangu, ndio ule utukufu ulionipa kwa sababu ulinipenda mbele ya kuumbwa kwa dunia.


Sisi tuna uhodari na tungependa zaidi kutoka katika mwili huu na kwenda kuishi pamoja na Bwana.


Maana ninasongwa na mambo mawili. Ninatamani kujiendea na kukaa pamoja na Kristo, maana hili ndilo jambo bora zaidi.


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda nitamupa ruhusa ya kula matunda ya muti wa uzima unaokuwa katika bustani ya Mungu!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ