Pilato alipokuwa amekwisha kuikaa kwa kuamua maneno, muke wake akamutumia ujumbe huu: “Usijiingize katika maneno ya mutu huyo mwenye haki, kwa sababu usiku niliteseka sana katika ndoto kwa ajili yake.”
Pilato akawaambia kwa mara ya tatu: “Alifanya ubaya gani? Mimi sikumwona na hata kosa moja linalomustahili kuhukumiwa kufa. Nitaamuru apigwe fimbo, na kisha nitamufungua.”
Pilato akamwuliza: “Ukweli ni nini?” Pilato alipokwisha kusema neno hili, akatoka tena inje na kuwaambia Wayuda: “Mimi sioni hata sababu moja ya kumuhukumu mutu huyu.
Mimi niliona kwamba hakufanya kitendo chochote cha kustahili kufa. Lakini kwa sababu yeye mwenyewe aliomba maneno yake yakatwe na Mufalme wa Roma, nilikusudia kumutuma kwake.
Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.
Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.
Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.