Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 23:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Halafu Yesu akasema: “Baba uwasamehe, kwa maana hawajui jambo wanalofanya.” Waaskari wakagawanya nguo zake kwa kuzipigia kura.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 23:34
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

‘Mumwambie Yosefu kwa ajili yangu: Tafazali uwasamehe wandugu zako makosa yao mabaya na maovu yote waliyokutendea.’ Sasa basi, tafazali usamehe uovu tuliokutendea sisi watumishi wa Mungu wa baba yako.” Yosefu alipopata ujumbe huu, akalia.


Nimebaki mifupa mitupu; waadui zangu wananiangalia na kunisimanga.


Kwa hiyo nitamugawanyia sehemu pamoja na wakubwa, atagawanya vitu vilivyotekwa pamoja na wenye nguvu. Alijitoa yeye mwenyewe hata kufa; aliwekwa kundi moja na watu wakosaji. Alizibeba zambi za watu wengi, akawaombea musamaha hao wakosaji.


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Ndiyo, Baba, hayo yote ni kutokana na mapenzi yako.


Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.


Kisha wakamutundika juu ya musalaba, wakagawanyana nguo zake kwa kuzipigia kura, kusudi wajue nguo gani kila mumoja atakazopaswa kutwaa.


“Baba, kama ukitaka, ninakuomba uniondolee mbali kikombe cha mateso. Lakini isikuwe mapenzi yangu ndiyo yafanyike, lakini yako.” [


“Ninawaombea wao; siwaombei watu wa dunia, lakini hao ulionipa, kwa sababu wao ni wako.


Yesu akamujibu: “Wewe hauna mamlaka yoyote juu yangu, isipokuwa tu yale uliyopewa na Mungu toka juu. Ni kwa hiyo, yule aliyenitoa kwako anabeba zambi kubwa zaidi.”


Lakini Paulo akalalamika kwa nguvu akisema: “Usijiue, kwa maana sisi wote tuko hapa!”


“Sasa wandugu zangu, ninajua kwamba ninyi na wakubwa wenu mumemutendea Yesu hayo yote pasipo kujua nini munayofanya.


Kisha akapiga magoti, akalalamika, akisema: “Bwana, usiwahesabie zambi hii.” Na nyuma ya kusema maneno haya, akakufa.


Mumwombe Mungu awabariki wale wanaowatesa; muwaombee baraka wala musiwalaani.


Hakuna hata mutawala mumoja kati ya watawala wa dunia hii aliyeelewa hekima ile. Kama wangeielewa wasingemutundika Bwana wa utukufu juu ya musalaba.


Tunasumbuka sana tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Wakati tunapotukanwa, tunabariki; wakati tunapoteswa, tunavumilia;


Ingawa zamani nilikuwa mwenye kumutukana, mwenye kumutesa na kumutendea kwa ukali, lakini amenihurumia, kwa sababu yote niliyofanya, niliyafanya kwa upumbafu kwa maana sikukuwa bado na imani.


Musirudishiane mabaya kwa mabaya au matusi kwa matusi, lakini muombeane baraka, kwa sababu Mungu aliahidi kuwabariki ninyi wakati alipowaita kumufuata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ