Lakini aliumizwa kwa sababu ya zambi zetu, alipondwa kwa sababu ya maovu yetu. Kwa kuazibiwa kwake sisi tumepata uzima; kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
Pilato akawaambia kwa mara ya tatu: “Alifanya ubaya gani? Mimi sikumwona na hata kosa moja linalomustahili kuhukumiwa kufa. Nitaamuru apigwe fimbo, na kisha nitamufungua.”
“Musiwahukumu wengine, na Mungu hatawahukumu ninyi. Musikuwe wenye kukatia wengine azabu, naye hatawaazibu ninyi. Muwasamehe wengine, na Mungu atawasamehe ninyi vilevile.
Lakini Paulo akawaambia wajumbe: “Wametupiga mbele ya watu wote bila kutusambisha, ijapokuwa sisi ni wanainchi wa Roma, na kisha wakatutia ndani ya kifungo. Na sasa namna gani wanataka kututosha kwa uficho? Haiwezekani! Wao wenyewe wafike kutufungua!”