Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 22:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Yesu akawatuma Petro na Yoane, akisema: “Mwende mututayarishie chakula cha karamu ya Pasaka.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 22:8
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yesu akamujibu: “Ukubali kufanya hivi sasa. Kwa maana ni kwa njia hii tutatimiza mambo yote yanayokuwa ya haki mbele ya Mungu.” Basi Yoane akakubali.


Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


Wakamwuliza: “Ni wapi unapotaka tuende tukitayarishie?”


Siku moja, na saa tisa ya muchana, Petro na Yoane walienda katika hekalu kwa wakati wa maombi.


Mutu huyo hakutaka kuachana na Petro na Yoane. Kwa hiyo watu wote wakashangaa sana na kukimbilia kwenye baraza la hekalu wanaloita La Solomono.


Yule kiwete alipowaona Petro na Yoane wakiingia ndani ya hekalu, akawaomba musaada.


Wajumbe wa Baraza Kubwa walishangaa sana kuona namna Petro na Yoane walivyosema bila woga na kujua kwamba walikuwa watu wasiojulikana na wasiokuwa na elimu. Wakatambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.


Lakini Petro na Yoane wakawajibu: “Muamue ninyi wenyewe, ni haki mbele ya Mungu kuwatii ninyi kuliko kumutii Mungu?


Mitume waliokuwa Yerusalema waliposikia kwamba wakaaji wa Samaria wamekubali Neno la Mungu, wakawatumia Petro na Yoane.


Basi Yakobo, Petro na Yoane, waliohesabiwa kuwa waongozi wakubwa, walitambua neema ile niliyojaliwa na Mungu wakatupatia mukono, mimi na Barnaba kuwa kitambulisho cha ushirika. Hivi tukapatana kwamba sisi tutakwenda kuhubiri watu wa mataifa mengine na wao watakwenda kuhubiri Wayuda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ