Asubui mapema, mara moja wakubwa wa makuhani wakafanya shauri pamoja na wasimamizi wa watu, walimu wa Sheria na wakubwa wote wa baraza. Wakamufunga Yesu, wakamupeleka na kwenda kumutoa kwa Pilato.
Na kulipokucha asubui mapema, wakamutosha Yesu kwa Kayafa na kumupeleka kwenye nyumba ya liwali. Lakini Wayuda wenyewe hawakuingia ndani ya nyumba ya liwali, kwa maana kwa njia ile wangejichafua na kutoweza kuwa tayari kula karamu ya Pasaka.
Hata Kuhani Mukubwa pamoja na baraza lote la wasimamizi wa watu wanaweza kushuhudia kwamba ninasema kweli. Nilipata hata barua toka kwao iliyoandikwa kwa ajili ya wandugu Wayuda wa Damasiki. Nikaenda kule kusudi niwafunge waamini waliokuwa kule na kuwaleta mpaka Yerusalema wapate kuazibiwa.